Na Jaala Makame Haji-
ZEC
Mgombea
wa Udiwani kupitia Chama cha Mapinduzi Bi Salama Rajabu Masinga amekuwa wa
kwanza kuchukuwa fomu ya uteuzi kugombea nafasi ya Udiwani katika Uchaguzi
Mdogo wa Wadi ya Kinuni unaotarajiwa kufanyika tarehe 28 Machi,2021.
Akizungumza
katika hafla ya uchukuaji fomu ya Uteuzi iliyofanyika Maisara katika Ofisi ya
Uchaguzi ya Wilaya Magharibi “B” Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Pangawe Suluhu
Ali Rashid alisema, Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar haitoandikisha Wapiga Kura
Wapya kwa ajili ya kushiriki katika Uchaguzi Mdogo huo na badala yake wapiga kura walioandikishwa
katika Daftari la Kudumu kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu 2020 ndio watakaohusika
kupiga Kura katika Uchaguzi Mdogo huo
Aidha,
Bwana Suluhu aliviomba vyama vyengine vya Siasa kujitokeza kuchukua fomu za
uteuzi ili viteuliwe na Tume kushiriki katika Uchaguzi kwa ngazi ya Uwakilishi
Jimbo la Pandani na Udiwani Wadi ya Kinuni
Naye,
Mgombea wa Udiwani kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi Salama Rajabu Masinga
aliahidi kuyafanyia kazi maelekezo aliyoelekezwa na Tume ya Uchaguzi katika
ujazaji wa fomu za uteuzi kwa kufuata Sheria na Kanuni za Uchaguzi.
Kwa
upande wake Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Pandani aliwataja Wagombea Wa
Uwakilishi waliochukuwa fomu za uteuzi kuwa ni Mohammed Juma Ali kwa tiketi ya
Chama cha Mapinduzi, Said Hamad Ali Demokrasia Makini, Prof. Omar Fakih Hamad
ACT Wazalendo na Ali Hamad Omar wa ADA TADEA
Mgombea
wa Uwakilishi Masoud Ali Said na Mgombea
wa Udiwani Kassim Ali Abdalla kupitia chama cha Wananchi CUF wanatarajiwa
kuchukuwa fomu za Uteuzi kesho tarehe 5 Machi, 2021 katika Ofisi ya Uchaguzi ya
Wilaya ya Wete saa tano asubuh na saa tisa alasiri Ofisi ya Uchaguzi Wilaya ya
Magharib “B” iliyopo Maisara Unguja
No comments:
Post a Comment