Habari za Punde

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe.Othman Masoud Amefungua Kongamano la Dawa za Kulevya Zanzibar.

Na.Talib Ussi Zanzibar.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeeleza haitoweza kufanikisha mpango wake wa ajira laki tatu kuwa Bila ya Vijana madhubuti wenye siha na afya njema, akili timamu na walioelimika, pamona waliosalimika na dawa ya kulevya.

Hayo aliyaeleza  Makamu wa kwanza wa rais Zanzibar  Othman Masoud Othman huko Ocien view wakati akifungua kongamano la Madawa ya kulevya ambalo limeshirikisha wananchi wa mikoa mitatu ya Unguja pamoja na kamati za ulinzi na usalama.

Alisema ili kufikia mpango  huo kuna haja ya   kuwaokoa vijana na janga la matumizi ya madawa ya kulevya na  kukuzaa ushiriki wao katika kujenga taifa kupitia sekta ya ajira

“Lakini hayo tutayafikia kama vijana wetu watakuwa na afya njema na uwezo wa kufanyakazi na hili tikishikrikiana linawezekana, “ alisema Makamu huyo.

Alisema kuwa  ili vijana waweze kuwa warithi watakaokuja kuendeleza mipango, mikakati na malengo ya maendeleo ya Zanzibar  kunahitajika ushiriki  wao wa moja kwa moja  katika miradi ya Uchumi wa Buluu nchini ambapo  hilo  hilo halitowezekana  pasina afya na sia njema.

Alifahamisha kuwa dawa za Kulevya ni janga la Kimataifa, ambapo  Zanzibanr haikunusurika kwani imeathiriwa kwa kiasi kikubwa na tatizo hilo.

Alieleza kuwa  Zanzibar inakisiwa kuwa na takribani ya watu 10,000 wanaotumia dawa za kulevya na kiasi kikubwa ya waathiriwa hao ni vijana.

“Idadi hii sio ndogo na athari yake ni kubwa zaidi kuliko tunavyofikiria, kwani matumizi haya yanachochea maradhi mbali mbali ambayo  hudhofisha nguvu kazi ya Taifa ambao ni vijana wetu” alisema.

Akifafanuwa athari za ziada zitokanazo na Madawa hayo Makamu huyo, kuwa matumizi ya madawa hayo husababisha maradhi mbali mbali ikiwemo,  Kensa, magonjwa ya akili, maambukizi ya Ukimwi kufikia 5.1%, homa ya Ini B – 8.4% , Ini C – 15.1%  sambamba maradhi ya kujamiiana yamefikia 0.2%,.

Makamu alibainisha kuwa hali hiyo inaonyesha kwa kiasi gani nguvu kazi ya vijana inavyoweza kupotea kwa kasi ndani ya visiwa vya unguja na Pemba na kuathiri uchumi wa Visiwa hivyo.

Kongamano hillo la siku moja limepanga kuwasilishwa mada tatu ikiwemo Mipango ya kuzuia na kupambana na uhalifu wa Dawa za Kulevya,  Kuimarisha Kinga ya msingi dhidi ya Dawa za Kulevya pamoja na  Kutatua changamoto za utumiaji na matendo ya Dawa za Kulevya.

“Ili tuweze kufanikiwa katika kuyatekeleza hayo, ni wajibu wa kila mmoja wetu kutoa mawazo yake juu ya mbinu bora zitakazosaidia kuleta matokeo chanya ikiwemo kuzifanyia kazi zile kesi za Dawa za Kulevya zinazochukua muda mrefu bila kumalizika, kuhakikisha wahusika wanachukuliwa hatua stahiki kwa mujibu wa sheria namba 9 ya mwaka 2009 na Sheria nyengine zinazofanya kazi pamoja” alisema Makamu.

Alisema kwamba endapo kila mmoja akitimiza wajibu wake katika kuyasimamia  hayo kwa uzalendo na kwa uadilifu mkubwa itasaidia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar yenye Mfumo wa umoja wa kitaifa  kujenga uchumi imara na kufikia malengo iliyojipangia kwani itaweza kupunguza gharama za kuwatibu vijana walioathirika na Dawa hizo.

Alisema azma ya Serikali ya Zanzibar  ni kuona wananchi wake wanaishi katika maisha mazuri bila ya biashara wala matumizi ya Dawa za Kulevya.

Pia kwa upande mwengine alisema  kuna jumla ya kesi  654 kwa mwaka 2018, kesi 503 kwa  mwaka 2019 na kesi 454  kwa mwaka 2020 Kwa mujibu wa taarifa za polisi, na kueleza kwamba huo  ni ushahidi tosha na  kuthibitisha kuwa dawa za kulevya zinaingizwa nchini zanzibar.

Aliwaomba washiriki wa kongamano hilo  pamoja na wananchi kwa ujumla kushiriki katika vita hivyo kwani wote ni wadau katika Mapambano ya dawa za Kulevya na siyo kuachia mtu mmoja au Taasisi moja.

Alisema vita ya Madawa ya kulevya ni kubwa mnoo na kufahamisha  moja ya silaha zake ni mashirikiano ya pamoja kuanzia ngazi ya jamii ambae itahitajika kutoa taarifa za uhalifu hadi Mahkama ambayo itatoa maamuzi katika kesi hizo.

Akitoa neno shukrani makamu wa kwanza wa rais, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharbi, Idrisa Kitwana ameeleza iko haja ya kuiongezea makali sheria iliyopo kuendana na wakati

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.