. Shafi Dauda (kushoto) na Baraka Kizuguzo ambaye ni Afisa Mashindano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu(TFF) wakichezesha droo ya upangaji wa makundi ya timu na ratiba ya mashindano ya Taifa CUP 2021.
Naibu
Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo. Mhe, Pauline Gekul akishuhudia droo ya
upangaji wa makundi ya timu na ratiba ya mashindano Taifa CUP 2021ambayo
yanatarajia kuanza Disemba 10, 2021 jijini Dar es Salaam. Kushoto Kaimu Katibu
wa Baraza la Michezo la Taifa. Bi Neema Msita, kulia Mkurugenzi wa Michezo.
Yusuf Omary Singo.
Naibu Waziri wa Utamaduni,
Sanaa na Michezo. Mhe, Pauline Gekul leo, Disemba 7, 2021 ameshuhudia
droo ya upangaji wa makundi ya timu na ratiba ya mashindano Taifa CUP 2021ambayo
yanatarajia kuanza Disemba 10, 2021 jijini Dar es Salaam.
Akizungumza katika tukio hilo amesema anamshukuru Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mhe, Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia
kurejesha mashindano hayo ambayo yalikuwa yamesimama kwa miaka kadhaa.
Aidha amesema mashindano ya mwaka huu yameboreshwa tofauti na yale ya awali.
Amesema maboresho hayo ni pamoja na kuingiza michezo
mitatu; soka kwa wanaume na wanawake, netiboli na riadha kwa wanaume na
wanawake ambapo awali ulikuwa mchezo mmoja tu wa soka.
Pia amesema mashindano haya yameshirikisha pande zote mbili za Tanzania ili kuwa na sura ya kitaifa
Ametoa rai kwa vyama vya michezo na mashirikisho kuja kwenye mashindano hayo ili kuona vipaji vya wachezaji ambao wanaweza kuwachukua kwenye vilabu vyao.
Akizungumzia dhana ya Taifa CUP amesema lengo la mashindano hayo ni kuwashirikisha wanamichezo kutoka mikoa yote nchini ambapo amesisitiza kuwa mashindano hayo yanasaidia kuleta umoja na mshikamano, kutoa ajira na
kuimarisha afya za wachezaji hao.
Akimkaribisha Mhe. Gekul kutoa hotuba fupi kabla ya kuchezesha droo hiyo Mkurugenzi wa Michezo nchini ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Maandlizi ya Taifa CUP, Yusufu Omary Singo amesema droo hiyo imechezeshwa kwa uwazi ili kuyafanya yawe wazi zaidi
No comments:
Post a Comment