Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa
Pili wa Rais Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi, Hamza Hassan
Juma akimkabidhi funguo na gari tano,
Mratibu wa TASAF Unguja, Makame Ali Haji,
Magari kutoka Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya
Matumizi ya Shughuli za TASAF
makabidhiano yaliyofanyika katika Ofisi
za TASAF, Mazizini. (PICHA NA OMPR)
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar
imehimiza umuhimu wa kulipa kodi kwa maendeleo ya wananchi wake ili kufikia
malengo iliyojiwekea.
Aidha,
imewataka watumishi kutoka sekta za umma na binafsi kudai risiti za mashine
wakati wote wanapofanya matumizi ya mahitaji yao kwa lengo la kunusuru fedha za
serikali zisipotee.
Akizungumza
kwenye hafla fupi ya makabidhiano ya gari tano kwa uongozi wa Mfuko wa
Maendeleo ya Jamii, TASAF huko ofisi za mfuko huo, Mazizini mjini Unguja,
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais, Sera na Uratibu na Baraza la
Wawakilishi, Hamza Hassan Juma alisema fedha zilizotumika kunununulia gari hizo
ni za serikali ya Jamuhuri ua muuungano wa Tanzania ambayo imekopa kutoka benki
ya dunia.
Alisema
serikali ndie inalipa fedha hizo, kupitia kodi wanazolipa wananchi, hivyo
aliwataka wananchi kudai risiti za mashine kila wanaponunua mahitaji yao.
“Tunaponunua
bidhaa, lazima tupatiwe risiti, tunapofanikiwa kudai risiti fedha
zinazopatikana kupitia risiti hizo zinakwenda kulipa deni la magari haya,
sababu hili ni deni la serikali, ni deni la wananchi”
“Kila
mtu akienda dukani kununa chochote lazima adai risiti ya mashine, na hili ni
agizo la serikali hata kwa watumishi wa umma kila wanapofanya malipo lazima wadai
risiti ili fedha hizo zikalipe deni la magari haya” alilisisitiza Waziri Hamza
Aidha,
alieleza fedha za serikali ni fedha za wananchi na kuongeza kuwa wananchi wanashiriki
kulipa mkopo huo kupitia kodi wanazozilipa wanapodai risiti.
Aliwataka
watumishi waserikali kuwa mfano mzuri kwa wananchi kwa kudai risiti za mashine
ili nao wawe wepesi kwa kudai risiti.
Akizungumzia
suala la ongezeko la mishahara kupitia ahadi ya Rais wa Zanzibar kwa watumishi
wa umma, Waziri Hamza alisema kudai risiti kwa bidhaa zinazouzwa ni kulipia
kodi kwa kudai risiti kutaisaidia serikali kukusanya mapato yanayokwenda kulipa
mishahara ya watumishi wake, kununuliwa nadawa na mahitaji mengine ya maendeleo
ya nchi.
Hata
hivyo alisema serikali imesamehe baadhi ya kodi kwa lengo la kuwapa ahuweni
wananchi wake na kutolea mfano kodi za mafuta.
Kwa
upande wa magari hayo Waziri Hamza aliueleza uongozi wa TASAF kwa kuwapa agizo
kutoka kwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, kwamba magari hayo
yakatumiwe kwa lengo lililokusudiwa na si vyenginevyo.
“Magari
haya yaendelee kuwahudumia wananchi na sio matumizi ya utashi wa mtu binafsi”
Nae
Katibu Mkuu Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais, Thabit Idarous Faina alisema
mbali ya kukabidhiwa gari tano kwa matumizi ya Unguja na Pemba na kuongeza kuwa
Mradi wa TASAF pia umekabidhiwa vifaa
vyengine vya kazi zikiwemo mashine za fotokopi ambavyo kwa mapaja na magari
hayo vinagharimu jumla ya milioni 394.
Akizungumzia
changamoto katika kuwafikiwa walengwa wa mradi wa TASAF, Katibu Faina alieleza
kwa kaiwaida walengwa hao wanatakiwa kufikiwa kila mwezi lakini kutokana na
changamoto ya awali ya usafiri walifikiwa kila baada ya miezi miwili.
Jumla
ya wanufaika 32,523 kwa Zanzibar wamefikiwa na mradi wa TASAF ambapo matarajio
ya kuzifikia elfu 50 kutoka shehia 388 za Unguja na Pemba kwa lengo la
kuwakwamua na ukali wa umasikini.
Imetayarishwa na kitengo cha habari
na mawasilinao, OMPR
No comments:
Post a Comment