Habari za Punde

Mabalozi Wanaokwenda Kuiwakilisha Tanzania watakiwa Kuitumia Diplomasia ya Kiuchumi kwa Kuzitafuta na Kuzileta Fursa za Uchumi

 

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amewataka Mabalozi wateule wanaokwenda kuwakilisha Tanzania nchi  za Zimbabwe, Zambia na Uholanzi kuitumia vyema Diplomasia ya     Kiuchumi kwa kuzitafuta na kuzileta Tanzania fursa za kiuchumi zilizoko kwenye nchi hizo ili ziweze kuisaidia nchi.

Mhe. Othman ameyasema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na Balozi  Simon Sirro anayekwenda  Zambia, Balozi  Luten General Metheu anayekwenda Zimbawe na Balozi Caroline Chipeta anayekwenda kuwakilisha Tanzania katika nchi Uholanzi.

Mhe. Makamu amesema kewamba katika nchi zote hizo wanazokwenda zipo fursa nyingi  za kiuchumi na kiutaalamu ambazo zinaaweza kuisaidia Tanzania kujiendeleza  zaidi kiuchumi iwapo mabalozi hao watafanya juhudi ya kuzileta nyumbani  na kuweza kusaidia nchi yao.

Amewaleza Mabalozi hao kwamba katika nchi za Tanzania  ikwemo Zanzibar zipo fursa nyingi  za kuchumi  hasa katika kukuza na kuendeleza sekta ya utalii , biashara na kilimo maeneo ambayo  hayajatumika ipasavyo na kwamba mabalozi hao ni vyema wakajitahidi kuifanya kazi ya kuzitangaza ili zitumike kuisaidia nchi.

Amesema nchi ya Zambia inauwezo nzuri wa kusindika bidhaa za nyama na kwamba utaalamu huo unaweza ukatumika kuisaidia Tanzania kuongeza thamani ya bidhaa hizo na kuwa na Tija zaidi kwa nchi kuliko ilivyo sasa.

Aidha amewaeleza mabalozi hao kwamba Zanzibar inakabiliwa na changamoto ya maji ya bahari kusogea katika maeneo ya kilimo na kuathiri ardhi za kilimo na kwamba nchi ya Uholanzi utaalamu wao unaweza kutumika kuisaidia Zanzibar katika kulikabili vyema tatizo hilo .

Mhe. Othman amekumbusha mabalozi hao kuzitumia vyema fursa zinazopatikana katika Mashirika ya Kikanda na Kimataifa ikiwemo shirika la Kimataifa wabunifu ( WIPO), ili teknlojia na ubunifu wao uweze kuwasaidia vijana wa Tanzania katika jitihada za kukuza uchumi na maendeleo yao na Taifa kwa jumla.

Naye Kiongozi wa Mabalozi hao IGP Mstaafu wa Tanzania Simon Sirro ameeleza kwamba maelekezo wanayoyapata kutoka kwa viongozi wakuu ni nyenzo muhimu katika kazi yao na kwamba watajitahidi kuyatumia na kuyafuata katika kutimiza lengo na wajibu waliopewa  kuiwakilisha vyama Tanzania kwenye nchi wanazokwenda.

Amesema kwamba yeye wenzake watajitahidi kuhakikisha kwamba wanafanya wajibu wao vizuri wa kuitangaza nchi na kushirikiana na watangulizi wao kupitia Diplomasia ya kiuchumi kukidhi matarajio ya taifa katika kuleta maendeleo.

 Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia kitengo cha Habari leo tarehe 22.09.22

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.