Habari za Punde

Balozi Adadi Rajab Awataka Wanafunzi wa Shule ya Muheza Muskim Kusoma kwa Bidii

KAMISHNA wa Tume ya Utumishi wa Umma nchini Balozi Adadi Rajab akizungumza wakati wa maafali ya shule ya Sekondari Muheza Muslim.

Na Oscar Assenga,MUHEZA

KAMISHNA wa Tume ya Utumishi wa Umma nchini Balozi Adadi Rajabu amewataka wanafunzi katika shule ya Sekondari Muheza Muslim kuhakikisha wanasoma kwa bidii ili wataalamu mbalimbali waweze kupatikana kupitia huko.

Balozi Adadi aliysema hayo wakati wa mahafali ya shule hiyo yaliyofanyika mjini Muheza ambapo alisema lazima wanapokuwa shuleni waweze kujiandaa na  kuzingatia nidhamu ,malengo na kusoma vizuri ili baadae waje kufanikiwa kupitia elimu.

Alisema kwamba  mitihani inahitaji maandalizi mazuri ili waweze kufanya vema hivyo hawana budi kuhakikisha wanajiandaa ili kuweza kufanya vizuri katika mitihani yao.

Katika Mahafali hayo Balozi Adadi aliendesha Harambee kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya maabara katika shule hiyo ambapo huku akihaidi kuendelea kushirikiana nao katika kuhakikisha wanapata mafanikio.

Kamishna huyo aliuomba uingozi wa shule kwamba hiyo maabara utakapo kamilika ipewe jina la Bahoza Laboratory ili kuwaenzi kwa juhudi kubwa ambazo wamezifanya kufanikisha maabara hiyo.

Hata hiyo Balozi Adadi alisema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu imefanya mambo makubwa na kuleta maendeleo huku akieleza fedha ambazo zinakuja zinatokana na kurudisha mahusiano ya na mataifa mengine ambayo yalikatika na ameyarudisha kwa kasi kubwa.

Alisema kutokana na kurejesha mahusiano hayo yamewasaidia kupata fedha nyingi za kujenga shule, maabara,barabara na kila Jimbo kuhakikisha maendeleo yanapatikana  ule ufufuaji wa mahusiano na  mataifa mengine.

Katika hatua nyengine Balozi Adadi aliitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini kuhakikisha wana buni  mbinu zinazoweza kudhibiti vitendo vya rushwa ya ngono nchini.

Balozi Adadi alisema kwamba vitendo vya rushwa ya ngono vimekuwepo na  Takukuru wamepewa jukumu la kudhibiti  vitendo hivyo ni wakati sahihi kuhakikisha wanakuja na mwarobaini wake.

Alisema kwamba wao wanapaswa kuona namna nzuri ya kubuni mbinu ambazo zinaweza kupelekea  kudhibiti badala ya kusubiri matukio yanatokea ndio waweze kuanza kupambana nayo.

" Haya mambo yapo kwa sababu kwenye vyuo hivyo ni jinsi ya vyombo vilivyo kabidhiwa kufanya kazi hiyo wanafanya nini ili kuweza kuondokana na tatizo hilo"Alisema Balozi Adadi.

Aidha alisema kwamba wanataka wanaofanya vitendo hivyo wakamatwe ili iweze kuwa fundisho kwa wengine wenye tabia za namna hiyo kuweza kubadilika hivyo suala hili lina umuhimu wake  hasa chombo ambacho kimepewa mamlaka ya kusimamia. 

Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Muheza Muslimu
KAMISHNA wa Tume ya Utumishi wa Umma nchini Balozi Adadi Rajab akigawa vyeti kwa wahitimu wa kidato cha nne  wakati wa maafali ya shule ya Sekondari Muheza Muslim 
KAMISHNA wa Tume ya Utumishi wa Umma nchini Balozi Adadi Rajab akigawa vyeti kwa wahitimu wa kidato cha nne  wakati wa maafali ya shule ya Sekondari Muheza Muslim 



Na Oscar Assenga,MUHEZA

KAMISHNA wa Tume ya Utumishi wa Umma nchini Balozi Adadi Rajabu amewataka wanafunzi katika shule ya Sekondari Muheza Muslim kuhakikisha wanasoma kwa bidii ili wataalamu mbalimbali waweze kupatikana kupitia huko.


Balozi Adadi aliysema hayo wakati wa mahafali ya shule hiyo yaliyofanyika mjini Muheza ambapo alisema lazima wanapokuwa shuleni waweze kujiandaa na  kuzingatia nidhamu ,malengo na kusoma vizuri ili baadae waje kufanikiwa kupitia elimu.

Alisema kwamba  mitihani inahitaji maandalizi mazuri ili waweze kufanya vema hivyo hawana budi kuhakikisha wanajiandaa ili kuweza kufanya vizuri katika mitihani yao.

Katika Mahafali hayo Balozi Adadi aliendesha Harambee kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya maabara katika shule hiyo ambapo huku akihaidi kuendelea kushirikiana nao katika kuhakikisha wanapata mafanikio.

Kamishna huyo aliuomba uingozi wa shule kwamba hiyo maabara utakapo kamilika ipewe jina la Bahoza Laboratory ili kuwaenzi kwa juhudi kubwa ambazo wamezifanya kufanikisha maabara hiyo.

Hata hiyo Balozi Adadi alisema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu imefanya mambo makubwa na kuleta maendeleo huku akieleza fedha ambazo zinakuja zinatokana na kurudisha mahusiano ya na mataifa mengine ambayo yalikatika na ameyarudisha kwa kasi kubwa.

Alisema kutokana na kurejesha mahusiano hayo yamewasaidia kupata fedha nyingi za kujenga shule, maabara,barabara na kila Jimbo kuhakikisha maendeleo yanapatikana  ule ufufuaji wa mahusiano na  mataifa mengine.

Katika hatua nyengine Balozi Adadi aliitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini kuhakikisha wana buni  mbinu zinazoweza kudhibiti vitendo vya rushwa ya ngono nchini.

Balozi Adadi alisema kwamba vitendo vya rushwa ya ngono vimekuwepo na  Takukuru wamepewa jukumu la kudhibiti  vitendo hivyo ni wakati sahihi kuhakikisha wanakuja na mwarobaini wake.

Alisema kwamba wao wanapaswa kuona namna nzuri ya kubuni mbinu ambazo zinaweza kupelekea 
 kudhibiti badala ya kusubiri matukio yanatokea ndio waweze kuanza kupambana nayo.

" Haya mambo yapo kwa sababu kwenye vyuo hivyo ni jinsi ya vyombo vilivyo kabidhiwa kufanya kazi hiyo wanafanya nini ili kuweza kuondokana na tatizo hilo"Alisema Balozi Adadi.

Aidha alisema kwamba wanataka wanaofanya vitendo hivyo wakamatwe ili iweze kuwa fundisho kwa wengine wenye tabia za namna hiyo kuweza kubadilika hivyo suala hili lina umuhimu wake  hasa chombo ambacho kimepewa mamlaka ya kusimamia.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.