Habari za Punde

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi Ameshiriki katika Kisomo cha Hitma na Dua Kumuombea Marehemu Dkt. Mwinyihaji Makame Mwadini Iliyofanyika leo Bweleo

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Wananchi wa Bweleo katika kisomo cha Hitma na Dua ya kumuombea Marehemu Dkt. Mwinyihaji Makame Mwadini kilichofanyika katika Msikiti wa Ijumaa Bweleo Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 23-10-2022, na (kulia kwa Rais) Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Khalid Ali Mfaume na (kushoto kwa Rais) Mwalimu Khamis.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi  Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi amejumuika na viongozi mbalimbali,waumuni wa dini ya kiislamu,familia pamoja na  wananchi wa Jimbo la Dimani katika Dua Maalum (Khitma) ya kumuombea Mwanasiasa Mkongwe wa Zanzibar Marehemu Dkt.Mwinyihaji Makame Mwadini aliefariki Alkhamis Usiku wa tarehe 20 Oktoba 2022 Nyumbani kwake  na Kuzikwa kijijini kwao Bweleo,Wilaya ya Magharibi ‘B’,Mkoa wa Mjini Magharibi.

Hitma hio ya kumuombea Marehemu Dkt Mwinyihaji Makame Mwadini imefanyika katika katika Msikiti Mkuu wa Ijumaa wa Bweleo ambapo Sheikh Mussa Ali Kirobo ndie alieongoza Dua hio (Hitma)ya kumuombea Marehemu Dkt.Mwinyihaji Makame Mwadini.

Katibu Mtendaji wa Afisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khalid  Ali Mfaume aliwasihi waumini  na wananchi waliojumuika katika Dua hio kuyakumbuka mema ya Marehemu ambayo aliyokua akiyatekeleza wakati wa Uhai wake huku akimuelezea kuwa Marehemu Dkt.Mwinyihaji Makame alikua Mtaratibu,Mwenye kumuheshimu kila mmoja,muungwana na ni mwenye kumsikiliza mtu haja zake. Huku akiongezea kuwa Mauti inatosha kuwa ni ukumbusho na mawaidha kwa kila mmoja. Akisisitiza kuwa Dunia sio yetu licha ya kupambwa na kila aina ya Mapambo mazuri.

Vile vile alimuombea dua Marehemu Mwenyezi Mungu amsamehe makosa yake na amjaalie awe miongoni mwa waja wema wa Mwenyezi Mungu.

Mara baada ya kukamilika kwa dua hio Sheikh Ibni Ahmed Haji alitoa shukrani kwa Rais wa Zanzibar Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi kwa kujumuika nao katika kumuombea Mzee wao,huku akisisitiza shukrani za dhati kwa Serikali nzima pamoja na Chama cha Mapinduzi kwa kuwa karibu na familia hio tokea msiba umetokea hadi kufikia siku hio ya Dua maalum na kuchukua nafasi hio kumuombea dua za kheri Rais Dk.Mwinyi katika kuiongoza Zanzibar.

Alhaj Dk.Mwinyi akiwa Msikitini hapo alipata muda wa kuwapa pole familia ya marehemu pamoja na kuwakabidhi Ubani.

Marehemu Dkt.Mwinyihaji Makame Mwadini katika Uhai wake alishika Nafasi mbalimbali za uongozi katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Chama cha Mapinduzi ikiwemo Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – Ikulu,Waziri wa Fedha na Mipango,Waziri wa Afya na Utawi wa Jamii pamoja na kuwa Mwakilishi wa kuachaguliwa na Wananchi katika Jimbo la Dimani tokea mwaka 2000 hadi 2020 na kuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi Taifa.

“Sisi sote ni wa Mwenyezi Mungu na kwake Tutarejea”.

Imetayarishwa na Idaya ya Mawasiliano

                          Ikulu Zanzibar.                          

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akijumuika na Wananchi wa Bweleo katika kisomo cha Hitma na Dua ya kumuombea Marehemu Dkt. Mwinyihaji Makame Mwadini kilichofanyika katika Msikiti wa Ijumaa Bweleo Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 23-10-2022, na (kulia kwa Rais) Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Khalid Ali Mfaume na Balozi Mohammed Ramia Abdiwawa  (kushoto kwa Rais) Mwalimu Khamis

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akishiriki kuitikia dua ya kuhitimisha kisomo cha Hitma ikisomwa na Sheikh Mussa Ali Kirobo.(hayupo pichani) kumuombea Marehemu Dkt. Mwinyihaji Makame Mwadini kilichofanyika katika Msikiti wa Ijumaa Bweleo Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 23-10-2022, na (kulia kwa Rais) Katibu Mtendaji wa Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh.Khalid Ali Mfaume na (kushoto kwa Rais) Mwalimu Khamis.

Wanafamilia na Ndugu wa Marehemu Dkt.Mwinyihaji Makame Mwadini wakiitikia dua ya kumuombea iliyofanyika katika Msikiti wa Ijumaa Bweleo Wilaya ya Magharibi "B"Unguja leo 23-10-2022.

Wananchi wa mbalimbali na wa Kijiji cha Bweleo wakiitikia Dua baada ya kumalizika kwa kisomo cha hitma ya kumuombea Marehemu Dkt.Mwinyihaji Makame Mwadini iliyofanyika katika Msikiti wa Ijumaa Bweleo Wilaya ya Magharibi "B"Unguja leo 23-10-2022.

Wananchi wa mbalimbali na wa Kijiji cha Bweleo wakiitikia Dua baada ya kumalizika kwa kisomo cha hitma ya kumuombea Marehemu Dkt.Mwinyihaji Makame Mwadini iliyofanyika katika Msikiti wa Ijumaa Bweleo Wilaya ya Magharibi "B"Unguja leo 23-10-2022.

Mwakilishi wa Familia ya Marehemu Mwinyihaji Makame Mwadini Sheikh.Ibni Ahamad Haji akizungumza na kutowa neno la shukrani baada ya kumalizika kwa kisomo cha Hitma na Dua ya kumuombea Marehemu Dkt.Mwinyihaji Makame Mwadini iliyofanyika katika Msikiti wa Ijumaa Bweleo Wilaya ya Magharibi "B" Unguja leo 23-10-2022.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akitowa mkono wa pole kwa Familia ya Marehemu Dkt.Mwinyihaji Makame Mwadini, baada ya kumalizika kwa kisomo cha Hitma na Dua ya kumuombea Marehemu iliyofanyika katika Msikiti wa Ijumaa Bweleo Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 23-10-2022




 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.