Habari za Punde

Mhe Othman ashiriki Hauli ya Maalim Seif Masjid Omar Bin khattab, Msumbiji




MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman , amejumuika na Viongozi, wafuasi  wa na Wanachama wa Chama cha Act- Wazalendo pamoja na waumini  wa Dini katika haluli ya kumuombea Dua aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar marehemu Maalim Seif Sharif Hamad.

Dua hiyo iliyofanyika katika Masjid Omar Bin khattab katika mtaa wa Msubiji ni kumbukumbu ya kutimia miaka miwili tangu kufariki kwa kiongozi  huyo mashuhuri mnamo tarehe 17 Februari mwaka 2021.

Marehemu Malim Seif alifariki Dunia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikolazwa kwa matibabu kwa kipindi cha takribani wiki mbali baada ya afya yake kodorora zaidi alipokuwa amelezwa awali kwa matibabu katika Hospitali ya Mnanzi mmoja.

Akitoa wasifu wa Kiongozi huyo baada ya kukamilika kwa dua hiyo Mjumbe wa Kamati Kuu ya ACT- Wazalendo Nd. Hassan Jani Masoud, amesema kwamba kiongozi huyo alikuwa na mwenendo bora na kuwa msamehefu kwa kila aliyemkosa.

Amesema kwamba maalim Seif aliwajali wanancho wote na hasa wanyonge na hakuwa mkachu wa tabia sambamba na kujitoa katika kutetea maslahi ya Zanzibar na watu wake bila kuchoka katika maisha yake yote.

 Mjumbe huyo wa Kamati Kuu amewataka wananchi wa Zanzibar kuishi na sifa ya maalim Seif kwa kuwa alikuwa ni mtu mstahamilivu, msamehevu na aliyejiweka katika dara la kati aliyeishi vyema na watu wa aina zote hata wale waliomkosa.

Aidha amesema kwamba maalimu seif alikuwa kiongozi  mwenye huruma aliefuata vigezo na maelekezo mema katika kusimamia na kuwaongoza wananchi na wafuasi wake jambo lilomfanya kupata mapenzi kwa watuwatu wengi ndani na nje ya Zanzibar.

Naye Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa ACT- Wazalendo Nd. Salim Biman kwa niaba ya Viongozi wawakuu wa Chama hicho amesema kwamba anawashukuru watu wote waliokusanyika katika maeneo mbali nchini kumuombea dua marehemu Maalim Seif Sharif Hamad.

Dua kama hiyo imesomwa katika misikiti mbali mbali ya Unguja na Pemba , Dar es Salama  na kwengineko kwa nia ya kumkumbuka na kumuombea kwa mwenyezimungu amsamhe makossa yake na amuweke mahali pema Peponi.

 

Mwisho.

Imetolewa na Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia Kitengo chake cha Habari leo tarehe 17.02.2023.


 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.