Habari za Punde

Wananchi Watakiwa Kuendelea Kushikamana Katika Mafunzo Yanayopatikana Mwezi Mtukufu wa Ramadhani - Masoud

Na.Mwandishi wa OMWKR. 

MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman amewataka wananchi kuendelea kushikamana na  mafunzo yanayopatikana katika mwezi mtukufu wa ramadhani kwa kufanyanyiana ihsani kwa wenye uwezo kuwasaidia wenye  kipato duni.

Mhe. Othman ametoa kauli hiyo, huko Mombasa Wilaya yas Magharib B alipokuwa akitoa majumbuisho ya zaira yake ya kuwatembelea wangonwa na wenye misiba kama ni ada inayofanywa kila mwaka ikiwa ni muendelezo wa mtangulizi wake marehemu  Maalim Seif Sharif Hamad.

Mhe. Othman ambaye pia ni Mkamu Mwenyekiti wa Chama cha ACT -Wazalendo amefahamisha kwamba ramadhani inatoa mafunzo  makubwa kwa waumini kuweza kushiakamana na kuendeleza mambo ya kheir na kwamba kusaidiana ni moja wapo ya mafunzo muhimu yanayopatikana katika mwezi mtukufuu wa mfungo wa Ramadhan.

Mhe. Makamu amesema kwamba pia waumini watumie mafunzo ya mwenzi mtukufu wa ramadhani kwa kusamehe na kusamehena katika masuala mbali mbali ya makossa yualiyotokea aili kwa pamoja ziweze kupatikana kheri za mola mumba.

Mhe. Othman amewataka wagonjwa kuendelea kuwa na subra licha ya mtiani wa maradhi yaliyowapata na kuwataka kufahamu kwamba maradhi ni mtihani kutoka kwa mola muumba kumkumbuka mja wake na kuwaombea kwa mwenyezimungu wapone haraka ili waweze kushiriki katika shughuli zao za kujitafutia riziki na ujenzi wa taifa.

Amefahamisha kwamba kuwatembelea wagonjwa kunajenga imani kwa anayetembelewa lakini pia ni ada inayotokana na dini  na kwamba waezee wamefuata miongozo hiyo hivyo ni vyema kwa pamoja kuiendeleza.

Mapema Mwenyekiti wa  ACT- Wazalendo Mkoa Magharib ‘B’ Kichama Ndugu Ali Juma amesema kwamba ziara hizo zinasaidia sana katika kujenga hamasa kwa jamii katika kuona kwamba viongozi wanashirikiana na kushikana vyema na wanaowaongoza katika jamii.

Mhe. Othman amemaliza ziara yake ya kuwatembelea wagonjwa na wenye misiba katika mikoa yote ya Unguja ambapo leo amemalizia katika majimbo ya wilaya ya Magharib ‘A’ na ‘B’ Unguja na na anatarajiwa kufanya ziara kama hiyo  kisiwani Pemba  mapema wiki ijayo.

Imetolewa na ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia kitengo chake cha habari leo tarehe 29.03.2023.u

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.