Habari za Punde

Mhe Othman ahimiza ujenzi wa matawi ya chama cha ACT majimboni

 

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Acti Wazalendo Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman aewataka wanachama wa  chama hicho kuendelea kushirikiana katika  kuunga mkono juhudi za pamoja za ujenzi wa matawi ya chama katika majimbo mbali mbali ili kuwa na ofisi rasmi za chama hicho.

Mhe. Othman ameyasema hayo kwa nyakati tofauti huko katika Kijiji cha Koani Kibonde Maji Jimbo la Tunguu na Ndijani Kiunga Ndege  Jimbo la Chwaka wilaya ya Kati Unguja aliposalimia wanananchi na wanachama wa chama hicho baada ya kuweka mawe ya msingi ya ujenzi wa matawi kwenye maeneo hayo.

Mhe. Othman ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar amesema kwamba chama ni taasisi muhimu  na kwamba juhudi za kuwepo ujenzi wa ofisini ni alama za chama katika kuendeleza juhudi za pamoja za kuimarisha taasisi na kuwa na mahala bora pa kufanyia kazi.

Amewataka wa wanachama wa chaka hiyo kuendelea kushirikiana na kujitolea kwa hali na mali katika kuunga mkono juhudi za ujenzi wa ofisi za Chama zinazoanzishwa  katika maeneo na majimbo mbali mbali.

Ametoa wito kwa   wananchama na wapenzi wa chama hicho kuendelea kujitolea katika kuimarisha uhai wa chama kwa kuendeleza ujenzi wa matawi mbali mbali na kwamba juhudi hizo zinaendelea kuungwa mkono na viongozi katika ngazi tofauti ili kuweza kufanikisha maelengo ya chama.

Mhe. Othman amefahamisha wanachama hao kwamba juhudi za pamoja ndio njia ya pekee itakayosaidia chama hicho kufikia malengo yake ya kuhakikisha kwamba wanasaidiana kwa pamoja katika kuleta maslahi bora ya Zanzibar ili kuweza kufikia lengo la kupatikana maendeleo ya Zanzibar.

Amewataka wanachama wa chama hicho kuendelea kushajiishana na kushikamana katika kuunga mkono juhudi mbali mbali zinazoanzishwa na wanachama na viongozi katika ngazi tofauti kwa maendeleo ya Zanzibar.

Naye Mwanasheria Mkuu wa ACT – Wazalendo ambaye pia ni waziri wa Biashar na Viwanda Zanzibar Mhe. Omar Said Shaaban amesema kwamba  ni muhimu kwa viongozi na wanachama kushirikiana katika kuendeleza jitihada za pamoja na kuimarisha chama.

Amesema kwamba viongozi mbali mbali wapo tayari  kujitolea kwa hali na mali kuungana na juhudi za wanachama katika kutekeleza jitihada za pamoja za kuleta maendeleo ya chama ikiwemo ujenzi wa ofisi  za matawi na majimbo ili kuleta uhai wa chama hicho.

Mhe. Othman yupo katika  katika  muendeleo wa ziara za kuetembelea mjaimbo mbali mbali katika mkoa wa kusini iliwa ni muendelezo wa kuhutubia mkitano ya hahdara katika majimbo mbali mbali Unguja na Pemba na  baadae atahutubia mkutano wa hadhara  wa chama hicho huko chwaka wilaya ya Kati Unguja.

Kitengo cha Habari

Ofisi ya Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar

30, Julai, 2023   

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.