MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi,
CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk.
Hussain Ali Mwinyi ameahidi kukisimamia chama hicho kiuchumi.
Aliyasema hayo, Ukumbi wa Baraza la
Wawakilishi, shehiya ya Bopwe Wete Pemba alipozungumza kwenye
Mkutano wa Mabalozi, wajumbe wa Halmashauri za majimbo, Wilaya na Mkoa wa Kaskazini
Pemba kichama ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya chama kisiwani humo.
Dk.
Mwinyi alisema ili chama kijiendeshe kiuchumi na kuwapatia maslahi watendaji
wake wa ngazi zote, lazima kijiekeze kiuchumi kwa kuwa na vitega uchumi vingi
kama sehemu ya mapato yake.
Pia
alieleza kufurahishwa kwake na rasilimali za chama alizozishuhudia kwenye ziara
zake za mikoa yote kichama Unguja na Pemba na kueleza kuzifanyia tathmini
kuangalia uwezekano wa ya kuziendeleza
kiuchumi ndani ya chama na baadhi yao kuziwekeza kwa sekta binafsi ili
kuziimarisha zaidi na kuongeza mapato ndani ya chama.
Pia, aliahidi kuwa na ofisi mpya za chama zenye
hadhi za juu pamoja na vitendeakazi vya ofisini zikiwemo, kompyuta na vifaa
vyote vya ofisi, ujenzi wa kumbi kubwa za mikutano zenye uwezo wa kubeba
mikutano mikuu ya chama kwa Unguja na Pemba.
Akizingumzia sekta ya maendeleo kisiwani Pemba hususani kuimaisha miundombinu ya barabara, bandari na viwanja vya ndege Pemba alisema amedhamiria kuifungua kiuchumi kwa kuruhusu ndege na meli za kimataifa kuingia Pemba na wawekezaji baada ya kufanywa marekebisho makubwa ya ujenzi wa miundombinu ya kisasa kwa bararabara, bandari ya Wete na kiwanja cha ndege.
Alieleza, tayari miradi mingi ya maendeleo
imekamilika ndani ya kipindi cha miaka miwili na nusu na kueleza juhudi zaidi
zimeelekezwa kuikamilisha miradi iliyobakia ikiwa ni utekelezaji Ilani ya
uchaguzi ya CCM, 2020- 2025.
Sambamba na hayo Dk. Mwinyi pia alikiagiza chama kutoa mafunzo kwa vongozi wepya ilikuwajengea uwezo katika utekelezaji wa kazi za chama hicho pamoja kukitaka kutayarisha mpango maalumu wa kuwatambulisha majukumu viongozi wapya, aidha, aliwaagiza kufanya vikao vya kikatiba ili kushughulikia mapema changamoto zinazokikabili chama kwaajili ya kuzitatua kwa wakati.
Naye, Naibu Katibu Mkuu CCM, Zanzibar, Mohamed Said Muhamed (Dimwa) alimueleza Makamu Mwenyekiti Dk. Mwinyi kwamba maagizo yote aliyayatoa ndani ya chama tayari yametekelezwa ikiwemo kuwapatia vitambulisho mabalozi wote wa CCM na watendaji wa ngazi zote kwaajili ya zoezi la kuanza kuwapatia maslahi yao.
Akizungumza kwenye mkutano huo, Mkuu wa Mkoa Kaskazini Pemba, Salama Mbaruok Khatib ndani ya kipindi cha miaka miwili na nusu cha utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM, 2020-2025 Kaskazini Pemba imepiga hatua kubwa kimaendeleo kwenye sekta zote zikiwemo maji elimu, afya miundombinu na michezo aliongeza ujenzi wa barabara mpya za nje na ndani unaendelea kwa kasi hubwana tayari serikali imewalipa fidia wananchi wa maeneo yote waliopitiwa na barabara.
Mapema
akizungumza kwenye Mkutano huo Mwenyekiti wa CCM, Mkoa Kaskazini Pemba, Mberwa Hamad Mberwa, alieleza hali ya amani, umoja na mshikamo kwa mkoa huo
bila kujali tofauti ya itikadi za vyama.
Aidha,
alieleza ushirikiano mkubwa wa viongozi wa chama na serikali kwa mkoa wa
kaskazini huo katika kutekeleza maendeleo na kueleza walivyokabiliana na kasoro
ndogo ndani ya chama chao.
Akiwa kwenye mwendelezo wa ziara yake kichama
Mkoa wa Kaskazini Pemba, Makamu Mwenyekiti Dk. Mwinyi pia alitembelea mali na
vitega uchumi vya chama ndani ya mkoa huo, ukiwemo ujenzi wa jengo la ghorofa
nne Micheweni litakalogharimu shilingi 1.187 bilioni litalohusisha maduka,
ofisi za chama na nyumba za biashara kama kitega uchumi cha chama
Pia Dk. Mwinyi alitembelea mali za chama za Jumuiya ya Wazazi shehia ya Machengwe Mkoa wa Kaskazini Pemba viwemo viwanja.
Ziara
ya Kaskazini Pemba imekamilisha ziara ya Makamu Mwenyekiiti Dk.Mwinyi ya kutembelea rasilimali za chama hicho zikiwemo
mali majengo na vitegauchumi vyake kwa mikoa yote mitano ya Unguja na Pemba
kichama.
IDARA
YA MAWASILIANO IKULU, ZANZIBAR
No comments:
Post a Comment