Habari za Punde

Zanzibar inahitaji mageuzi - Mhe Othman

 

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha ACT –Wazalendo Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba Zanzibar inahitaji kuingia katika Mageuzi yakayofanywa kwa  kuzingatia Amani ili nchi iendelee kuendeshwa kwa kuzingatia  mahitaji ya wananchi wenyewe wanavyotaka.

Mhe. Othman ambaye Pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, ameyasema hayo huko Chumbuni Wilaya ya Mjini Unguja alipozungunza katika Mkutano wa hadhara wa chama hicho akiwa katika mfululizo wa mikutano mbali mbali yenye dhamira ya kuelezea ahadi ya chama hicho kwa wananchi.

Amefahamisha  kwamba hatua hiyo ni muhimu kwani  itasaidia nchi  iendeshwe kwa mujibu wa maono  viongozi wa chama na wananchi wanavyotaka  wenyewe  ikiwa ni pamoja na kuzingatia haki ya kuchagua kiongozi na pia kuwa na uwezo wa kuwawajibisha na chama kiendelee kazi ya kuichunga na kuisimamia serikali.

Amesema kwamba hakuna nchi yoyote duniani inayoweza kuendelea na kupiga hatua iwapo wananchi hawana uwezo na mamlaka ya kuwachagua na kuwawajibisha viongozi wao  waliowachagua wanaoshindwa kuwajibika  kulingana na mwatakwa  ya wananchi kwa mujibu utaratibu .

Ni busara viongozi wa serikali kuwa na utaratibu wa kujisema wenyewe jambo litakalosaidia  kuwepo utamaduni wa utakaojengwa ndani ya chama kutimiza ahadi walizoziweka kwa wananchi kwa kuichunga serikali.

Amesema kwamba ni jambo muhimu kuwepo kwa muungano wenye kuzingatia haki  katika mashirikiano  ya kusimamia masuala mbali mbali yanayofanywa ikiwa ni pamoja na kuwepo uwezo wa kupanga kodi kwa mujibu wa hali ya uchumi wa Zanzibar bila kuwepo vizuizi ama vikwazo vinavyotokana na mashirikiano ya muungano uliopo.

Akizungunzia Rasilimali ya mafuta na gesi asilia amesema kwamba chini ya mfumo wa muungano uliopo Zanzibar haina  mamlaka ya kisheria kuweza kuchimba  mafuta kwa kuwa sharia inayosimamia rasilimali hiyo ndivyo inavyoeleza hadi sasa.

Amefahamisha kwamba ni vyema rasilimali ya gesi asilia na mafuta zikazingatiwa kama rasilimali za dhahabu ni  mali ya upande ilipo   badala ya zile zilioko Tanzania Bara kuwa hazihusiki na Zanzibar lakini ya mafuta na gesi iliytopo Zanzibar kufanywa kwamba ni ya muungano.

Amewataka wananchi kuendelea kushirikiana na kushikamana kwa kukiunga mkono chama hicho kwa kuwa kina maono ya kutafuta maendeleo ya kweli kwa wananchi wa Zanzibar .

Aidha amewataka wananchi wote ambao hawana Kitambulisho cha Manzibari mkaazi kuhakikisha kwamba wanafanya juhudi za kujiandikisha ili waweze kupata haki yao hiyo muhimu ambayo inaambatana na suala la kuwa mpiga kura.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Chama hicho Nassor Ahmed Mazuri amesema kwamba wananchi wanapaswa kushirikiana kukiunga mkono chama hicho kuendelea kuwa chama imara ambacho  kimejidhatiti katika kuleta mageuzi  yatakayaosaidia  kuondoa matatizo mbali mbali ya umasikini na ya kijamii.


Kitengo cha habari

Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar

23, Julai, 2023.

 

                                                                                                       

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.