Habari za Punde

Ziara ya Kamati ya Baraza la Wawakilishi Ofisi ya Makamu wa Rais Dodoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Dkt. Selemani Jafo akimuongoza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hamza Hassan Juma kuwasili katika Ofisi za Makamu wa Rais zilizopo Mtumba Jijini Dodoma muda mfupi baada ya kutembelea eneo la mradi wa ujenzi wa Majengo ya Taasisi za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika Eneo la Mahoma Makulu, Mkoani Dodoma tarehe 21 Agosti, 2023. 

Wajumbe wa Kamati ya Sheria, Utawala Bora na Idara Maalum za SMZ wa Baraza la Wawakilishi wakipokelewa na wenyeji wao Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Selemani Jafo na Naibu Waziri wa Ofisi hiyo, Mhe. Khamis Hamza Khamis mara baada ya kuwasili wakati wa ziara yao ya kutembelea Ofisi za Makamu wa Rais zilizopo katika Mji wa Serikali Mtumba Dodoma jana Jumatatu (Agosti 21, 2023)

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis katikati akiteta jambo na Mkurugenzi Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa Shughuli za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Bw. Khalid Bakar Amran wakati wa ziara ya wajumbe wa Kamati ya Sheria, Utawala Bora na Idara Maalum za SMZ wa Baraza la Wawakilishi waliotembelea eneo la mradi wa ujenzi wa Majengo ya Taasisi za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika Eneo la Mahoma Makulu, Mkoani Dodoma jana Jumatatu (Agosti 21, 2023).

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hamza Hassan Juma (kushoto) akizungumza jambo wakati wa ziara ya ya wajumbe wa Kamati ya Sheria, Utawala Bora na Idara Maalum za SMZ wa Baraza la Wawakilishi waliotembelea eneo la mradi wa ujenzi wa Majengo ya Taasisi za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika Eneo la Mahoma Makulu, Mkoani Dodoma jana Jumatatu (Agosti 21, 2023). Wa pili kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Selemani Jafo.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Selemani Jafo akizungumza jambo wakati wa kikao baina ya Viongozi na Watendaji wa Ofisi hiyo na Wajumbe wa Kamati ya Sheria, Utawala Bora na Idara Maalum za SMZ wa Baraza la Wawakilishi waliotembelea Ofisi hiyo tarehe 21 Agosti, 2023.

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Khamis Hamza Khamis akizungumza jambo na Wajumbe wa Wajumbe wa Kamati ya Sheria, Utawala Bora na Idara Maalum za SMZ wa Baraza la Wawakilishi mara baada ya kumalizika kwa kikao baina yao katika Ofisi za Makamu wa Rais, Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma tarehe 21 Agosti 2023.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hamza Hassan Juma (kushoto) wakati wa kikao na wa Wajumbe wa Kamati ya Sheria, Utawala Bora na Idara Maalum za SMZ wa Baraza la Wawakilishi mara baada ya kumalizika kwa kikao baina yao katika Ofisi za Makamu wa Rais, Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma tarehe 21 Agosti 2023.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Selemani Jafo (katikati) na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hamza Hassan Juma (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na  Wajumbe wa Kamati ya Sheria, Utawala Bora na Idara Maalum za SMZ wa Baraza la Wawakilishi mara baada ya kumalizika kwa kikao baina yao katika Ofisi za Makamu wa Rais, Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma tarehe 21 Agosti, 2023.

 

(PICHA NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS)

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.