Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitunukiwa Shahada
ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa) na Makamu Mkuu wa Chuo
Kikuu cha Jawaharlal Nehru Profesa Santishree Dhulipudi Pandit kwenye
hafla iliyofanyika New Delhi nchini India tarehe 10 Oktoba, 2023. Rais Samia ni
Mwanamke wa Kwanza kutunukiwa Shahada hiyo ya Heshima na Chuo hicho nchini
India. Ni Viongozi wawili tu ambao wametunukiwa Shahada hiyo ya Heshima akiwemo
Rais wa Urusi Mhe. Vladmir Putin pamoja na Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Japan
Hayati Shinzo Abe
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na
viongozi pamoja na wageni mbalimbali mara baada ya kutunukiwa Shahada ya
Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha
Jawaharlal Nehru kwenye hafla iliyofanyika New Delhi nchini India tarehe 10
Oktoba, 2023.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye hafla
ya
kutunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru, New Delhi nchini India tarehe 10 Oktoba, 2023.
Wanafunzi wa Vyuo Vikuu mbalimbali nchini India wakiwa kwenye hafla ambayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alitunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru, New Delhi nchini humo tarehe 10 Oktoba, 2023.
Walimu wa Chuo Kikuu cha Jawaharlal Nehru kilichopo New Delhi nchini India wakiwa kwenye hafla ambayo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alitunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Falsafa (Doctorate Honoris Causa) na Chuo hicho tarehe 10 Oktoba, 2023
No comments:
Post a Comment