Katika Hafla hiyo iliyopambwa kwa Kasidah na Milango ya Maulid ilitanguliwa na Dua ya kuwarehemu wazee waliotangulia mbele ya haki.
Akitoa Salamu zake katika hafla hiyo Mhe. Hemed amewataka wazazi na walezi kuwasimamia watoto kupata elimu itakayowasaidia kumjua Mola wao na kujua mafundisho ya Dini yao aliyokuja nayo Mtume Muhammad (S.A.W)
Amesema elimu bora na yenye manufaa hupatikana kwa kutanguliza nidhamu na adabu njema hatua ambayo itasaidia kuzalisha Viongozi bora watakaolisimamia Taifa wakiwa na hofu ya Mungu.
Sambamba na hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar amesisitiza suala la umoja na mshikamano katika jamii na kueleza kuwa ni wajibu wa kila mmoja kuhakikisha anasaidia jamii hasa makundi maalum ikiwemo Mayatima, wajane, wazee na wenye ulemavu hatua ambayo itasaidia kuongeza mapenzi katika Jamii.
……………………………..
Abdulrahim Khamis
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
10/10/2023
No comments:
Post a Comment