Habari za Punde

Rais Samia Suluhu Hassan ahitimisha ziara yake ya Kitaifa nchini Zambia



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Spika wa Bunge la Zambia Mhe. Malungo Chisangano mara baada ya kuwasili Bungeni hapo Lusaka nchini Zambia tarehe 25 Oktoba, 2023.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama pamoja na mwenyeji wake Rais wa Zambia Mhe. Hakainde Hichilema wakati wa Wimbo wa Taifa wa Tanzania na Zambia ukiimbwa mara baada ya kuhitimisha ziara yake ya Kitaifa ya Siku tatu nchini humo tarehe 25 Oktoba, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikagua Gwaride la Heshima wakati akihitimisha ziara yake ya Kitaifa ya Siku tatu nchini Zambia tarehe 25 Oktoba, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa pamoja na mwenyeji wake Rais wa Zambia Mhe. Hakainde Hichilema wakati wakielekea kuzungumza na Waandishi wa Habari katika Ikulu ya Lusaka nchini Zambia tarehe 25 Oktoba, 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na mwenyeji wake Rais wa Zambia Mhe. Hakainde Hichilema katika Ikulu ya Lusaka wakati akihitimisha ziara yake ya Kitaifa ya Siku tatu nchini humo tarehe 25 Oktoba, 2023.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu akiwashukuru Wabunge wa Bunge la
Zambia mara baada ya kuwahutubia tarehe 25 Oktoba, 2023. Rais Samia ni Rais wa Kwanza Mwanamke kulihutubia Bunge lililopo Lusaka nchini Zambia.

Rais wa Jamhuri ya Muungano waTanzania Mhe. Samia Suluhu akihutubia Bunge la Zambiawakati akihitimisha Ziara yake ya Kitaifa nchini humo tarehe 25 Oktoba, 2023. Rais Samia ni Rais wa Kwanza Mwanamke kulihutubia Bunge hilo lililopo Lusaka nchini Zambia.



 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.