Amesema, amekusudia kuikamilisha kwa vitendo
Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2020 – 2025 kwa miaka miwili iliyobakia ya
uongozi wake na kuikamilisha miradi mkikubwa ya kimkakati ya Bandari
Jumuishi ya Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja, barabara za kutulia na kurukia
ndege pamoja na jengo kubwa la abiria katika uwanja wa ndege wa Pemba
vinavyotarajiwa kugharimu zaidi ya dola za Marekeni milioni 400.
Dk. Mwinyi ambae ni Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha
Mapinduzi, CCM- Zanzibar aliyasema hayo, viwanja vya Maisara Suleiman
Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi, alipozungumza na Wazanzibari kwenye
maadhimisho ya miaka mitatu ya uongozi wake, tokea alipoingia madarakani
kuiongoza awamu ya nane ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, mwezi Novemba
mwaka 2020.
Pia, Rais Dk. Mwinyi amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Dk. Samia Suluhu Hassan kwa mchango mkubwa alioutoa kwa maendeleo ya Zanzibar na
kuongeza kuwa hatua ya maendeleo iliyofikiwa
ndani ya visiwa vya Unguja na Pemba kuna mkono wa Rais Dk. Samia.
Akizungumzia suala la amani, umoja na mshikamano, Rais Dk. Mwinyi alisema
maendeleo makubwa yaliyofikiwa Zanzibar ndani ya kipindi cha miaka mitatu ya
uongozi wake, yametona na juhudi kubwa ya wananchi wa Zanzibar, kuendelea kuidumisha
amani iliopo, umoja na mshikamano wao, umetoa fusra nzuri ya kutendeka
mafanikio yote hayo.
Aidha, Rais Dk. Mwinyi aliahidi kuongeza tena kasi ya maendeleo kwa
kipindi cha miaka miwili iliyobakia. Pia aliwapongeza Umoja wa Wanawake
Tanzania, (UWT) kwa kazi kubwa wanayoifanya nchi nzima, kukagua utekelezaji wa Ilani
ya CCM na miradi ya Maendeleo Tanzania bara na visiwani.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mwenyeketi
wa UWT Taifa, Merry Chattanda alipongeza juhudi kubwa ya mafanikio iliyofikiwa
na awamu ya nane ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwenye sekta zote za maendeleo
ikiwemo ujenzi wa barabra, Skuli, hospitali 10 za wilaya na moja ya mkoa iliyokamilishwa
kwa miundombinu na vifaa vya kisasa, ongezeko la ajira kwa vijana kupitia sekta
za ujenzi wa miundombinu, utalii, ujasiriamali, biashara na kilimo cha
umwagiliji wa mpunga, hali aliyoielezea matarajio ya Zanzibar kujiwekea akiba
ya chakula.
Pia, Chattanda alimpongeza Rais. Dk.
Mwinyi kwa kufanikiwa kuwakomboa wanawake wa Zanzibar dhidi ya changamoto cha
maji safi na salama kwa kuwajengea visima vikubwa vya maji, Unguja na Pemba pamoja
na kuwasambazia mabomba, kuwawekea usafiri wa haraka baharini kisiwani Pemba.
Aidha, Chattanda alisifu mchango mkubwa
unaotolewa na Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation
kupitia Mwenyekiti wake wa Bodi, Mama Mariam Mwinyi, Mke wa Rais wa Zanzibar kwa
kuwezesha kinamama wengi wakulima wa mwani na kuwajengea kiwanda kikubwa cha
kusarifu mwani, eneo la Chamanangwe, Pemba.
Mapema, akiwasilisha salamu za Chama
cha Mapinduzi viwanjani hapo, Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Bara, Abdul
Rahman Kinana aliwasihi Wazanzibari kuendelea kuidumisha amani na mshikano uliopo
baina yao na kuendelea kushirikiana na viongozi wao wa Serikali kuijenga Zanzibar.
Sherehe za maadhimisho ya miaka mitatu ya mafanikio ya awamu ya nane ya Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar, zilliandaliwa na kufanikishwa na Jumuiya ya CCM ya Umoja
wa Wanawake, Tanzania (UWT)
IDARA YA MAWASILIANO, IKULU ZANZIBAR.
No comments:
Post a Comment