Habari za Punde

Matokeo ya Sensa ya watu na makaazi mwaka 2022 yashushwa ngazi ya mikoa

Mtakwimu Mkuu wa Serikali Salum Kassim Ali akizungumza wakati wa kikao cha usambazaji na matumizi ya matokeo ya viashiria vya sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022 ngazi ya Mkoa huko Polisi Ziwani Mjini Unguja
Kamisaa wa Sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022 Tanzania Zanzibar Balozi Mohammed Haji Hamza akizungumza katika kikao cha usambazaji na matumizi ya matokeo ya viashiria vya sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022 ngazi ya Mkoa huko Polisi Ziwani Mjini Unguja
-Baadhi ya Masheha na Madiwani wakifuatilia kikao cha usambazaji na  matumizi ya matokeo ya viashiria vya sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022 ngazi ya Mkoa huko Polisi Ziwani Mjini Unguja


Na Fauzia Mussa ,   Maelezo

 

Mkoa wa Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe Idrissa Kitwana Mustafa  amewataka Watendaji wa ngazi za Wadi na Shehia kuyatumia matokeo ya Sensa ya watu na makaazi katika  kuleta maendeleo kwenye maeneo yao.

Akizungumza na Masheha na Madiwani wakati akifungua kikao cha usambazaji na matumizi ya matokeo ya viashiria vya Sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022 huko Polisi Ziwani Mkuu huyo  alisema endapo matokeo hayo yatatumika vizuri jamii itaweza kupanga mipango ya maendeleo katika sekta mbalimbali.

Aidha alisema Takwimu ya idadi ya watu itasaidia katika kuweka rasilimali ambazo zinatumika katika kukuza Uchumi wa Taifa na kupatikana kwa huduma za jamii kwa urahisi hivyo aliwataka  Viongozi hao  kutumia matokeo hayo katika ugawaji wa rasilimali kwa lengo la kuleta maendeleo Nchini.

 

Sambamba na hayo alitoa wito kwa Masheha na Madiwani kuwa Mstari wa mbele katika kufikisha taarifa hizo kwa jamii  ili kusaidia Serikali katika kutoa huduma sahihi  kwa wananchi.

 

Kwa upande wake Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar Salum Kassim Ali alisema Matokeo ya Sensa ni Muhimu kwani yanasaidia  kupanga, kusimamia pamoja na kubadilisha maisha ya Wananchi.

 

"Takwimu ya idadi ya watu itasaidia katika kusimamia mchakato wa kutoa huduma kwa Wananchi kwa lengo la kupata Maendeleo katika Nchi" alisema Mtakwimu  huyo

Alisema taarifa  zinazotolewa na Wananchi ndizo  zinazoiwezesha Serikali kubadilisha hali za Wananchi kwa kuwaletea Maendelo,hivyo  kuna kila sababu ya Wananchi kupatiwa  uwelewa wa umuhimu wa kutoa taarifa sahihi ili kueka mipango madhubuti katika upatikanaji wa huduma ikiwemo huduma za Afya.

Kwa upande wake kamisaa wa Sensa anaefanyia kazi zake Zanzibar Balozi Hamza Haji Hamza amesema kwa mujibu wa matokeo ya Sensa ya watu na makaazi ya mawaka 2022 imeonesha kuwa Mkoa wa Mjini Magharibi una idadi kubwa ya wakaazi ukilinganisha na mikoa mingine ya Zanzibar.

 

Hata hivyo aliwapongeza Masheha kwa kufanikisha kazi ya sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022  kuanzia matayarisho hadi kupatikana kwa matokeo mazuri.

Katika kikao hicho mada mbalimbali ziliwasilishwa ikiwemo matokeo muhimu ya baadhi ya Viashiria vya kiuchumi ,Kijamii na mazingira vitokananvyo na sensa ya watu na makaazi

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.