Habari za Punde

Nchi za SADC Zampongeza Rais Samia kwa Maono Yake Katika Usimamizi wa Misitu ya Miombo

 

Rais wa Jamhuri ya Watu wa Msumbiji, Mhe.Filipe Jaciton Nyusi akizungumza katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo  jijini Washington DC nchini Marekani leo Aprili 18,2024.

Nchi wanachama za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Southern African Development Community-SADC) zimempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maono yake katika usimamizi na uhifadhi wa misitu miombo hasa katika  kuhama kutoka kwenye matumizi ya nishati chafu kuelekea nishati safi ifikapo mwaka 2030.

Kauli hiyo imetolewa leo Aprili 18,2024 na Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) katika Mkutano wa Kimataifa unaohusu Misitu ya Miombo jijini Washington DC nchini Marekani.

“Kikubwa nchi zimeweza kumpongeza Rais wetu Dkt. Samia  Suluhu Hassan kwa namna ambavyo amekuwa akitoa maelekezo mbalimbali kwetu sisi kama Wizara na Sekta  katika kuhakikisha kwamba misitu ya miombo inalindwa  kwa nguvu kubwa, na kwa namna ambavyo amechukua uamuzi thabiti wa kuhakikisha kwamba inapofika mwaka 2030 zaidi ya asilimia 80 ya wananchi watakuwa wameachana na matumizi wa kuni na mkaa na watakuwa wamejielekeza katika nishati safi ya kupikia” Mhe. Kairuki amesisitiza.

Amesema kuwa misitu ya miombo nchini Tanzania katika ukanda wa kusini imekuwa ikikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uharibifu wa misitu ikiwemo uharibifu wa vyanzo vya maji, ukataji miti hovyo lakini Rais Samia amekuwa na jitihada mbalimbali kama Taifa kuhakikisha inalindwa kwa nguvu kubwa.

Aidha, amefafanua kuwa kupitia mkutano huo, nchi za SADC zimeweza kupata wafadhili  ambao wameanza kuonesha nia ya kusaidia mpango wa utekelezaji wa Azimio la Maputo la mwaka 2022 kuhusu ulinzi na uendelezaji wa misitu ya miombo.

Amesema lengo la Mkutano huo  ni kuona namna ya kuendeleza Azimio la Maputo katika kulinda na kuendeleza Misitu ya Miombo ambapo Tanzania ina zaidi ya  asilimia 93 ni Misitu hiyo yenye  aina ya spishes zaidi ya 8500, inatunza wanyamapori , miti na ina faida za kiuchumi na kijamii kwa upande wa masuala ya kilimo, upatikanaji wa dawa, chakula , vyanzo vya maji na huduma nyingine za msingi

Naye, Kamishna Uhifadhi wa Wakala ya Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Prof. Dos Santos Silayo  amesema kuwa kupitia mkutano huo nchi za SADC zimekuwa na majadiliano kuhusu kutafuta namna ya kushirikiana baina ya  nchi hizo na wadau mbalimbali wa maendeleo katika kupata rasilimali fedha, na kukuza ujuzi na utaalamu kwa ajili ya kuaidia uhifadhi wa misitu hiyo.

Amoengeza kuwa kongamano hilo limehitimishwa na hotuba ya Rais w Jamhuri ya Watu wa Msumbiji, Mhe.Filipe Jaciton Nyusi ambapo amesisitiza umuhimu wa nchi hizo kushirikiana katika kubadilishana taarifa , kukabiliana na masuala ya uharibifu wa mifumo ya ikolojia ya miombo hususan biashara haramu za mazao ya misitu na wanyamapori katika ukanda wa SADC.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki, Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Deusdedith Bwoyo amesema kuwa mkutano huo ni muhimu sana wa kuweza kuzungumza kwa pamoja changamoto za misitu ya miombo kwa nchi wanachama 11 za ukanda wa SADC na umekuja na majibu ya kuendeleza misitu ya miombo.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) (kulia) akiwa na baadhi ya Mawaziri wa nchi za SADC katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo jijini Washington DC nchini Marekani leo Aprili 18,2024.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb) akizungumza katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo  jijini Washington DC nchini Marekani 
Baadhi ya washiriki wa mkutano kutoka nchi mbalimbali wakipiga makofi baada ya kikundi cha burudani cha ngoma za asili kutumbuiza katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo uliofanyika  jijini Washington DC nchini Marekani leo Aprili 18,2024.
Rais wa Jamhuri ya Watu wa Msumbiji, Mhe. Filipe Jaciton Nyusi (katikati) akifuatilia mawasilisho kuhusu misitu ya miombo kutoka kwa wawakilishi wa nchi za SADC katika Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo  jijini Washington DC nchini Marekani leo Aprili 18,2024. Kushoto kwake ni Waziri wa Ardhi na Mazingira wa Msumbiji, Mhe.Ivete Maibaze na Balozi wa Umoja wa Afrika nchini Marekani, Mhe. Hilda Suka-Mafdze (kulia).
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mhe. Timotheo Mnzava (Mb) na baadhi ya washiriki wakifuatilia Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo uliofanyika  jijini Washington DC nchini Marekani leo Aprili 18,2024.

Rais wa Jamhuri ya Watu wa Msumbiji, Mhe.Filipe Jaciton Nyusi (wa tatu kutoka kulia) katika picha ya pamoja na Mawaziri wawakilishi kutoka nchi za SADC walioshiriki Mkutano wa Kimataifa kuhusu usimamizi endelevu wa misitu ya miombo jijini Washington DC nchini Marekani leo Aprili 18,2024. Kushoto kwake ni Waziri wa Ardhi na Mazingira wa Msumbiji, Mhe.Ivete Maibaze na Balozi wa Umoja wa Afrika nchini Marekani, Mhe. Hilda Suka-Mafdze (kulia). Katikati ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Angellah Kairuki (Mb).

 

 

 

 


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.