Habari za Punde

MKURUGENZI Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa habari za Mazingira Tanzania (JET) John Chikomo, akizungumza na viongozi wa eneo la Makuyuni Wildlife Park, wakati wa ziara ya waandishi wa habari JET, walipotembelea eneo hilo na kuona uhalisiwa wa wanyamapori, ikiwa ni utekelezaji wa Mradi wa USAID Tuhifadhi Maliasili unaotekelezwa na JET.

(PICHA NA ABDI SULEIMAN, ARUSHA)

Na. Abdi Suleiman - ARUSHA.

AFISA Utalii Makuyuni Wildlife Park Chacha 

Maramba Masase, amesema kuwa eneo la Makuyuni 

Wildlife Park ni lango kuu la utalii Arusha, kwa 

watalii wanaokwenda hifadhi mbali mbali kuangalia 

Wanyama.

Alisema eneo la Makuyuni lipo kilomita 115 kutoka uwanja wa 

ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro na kilomita 71 kutoka jiji 

la Arusha, ikizingatiwa eneo hilo lipo katika barabara kuu ya Arusha kwenda hifadhi mbali mbali.

Akizungumza na waandishi wa habari za mazingira Tanzania 

(JET), walipofika kujionea mazingira ya eneo hilo, ikiwa ni 

utekelezaji wa mradi wa USAID Tuhifadhi Maliasili 

unaotekelezwa na JET.

Alisema eneo hilo lipo katika lengo la taifa la kuongeza idadi 

ya watalii Tanzania, pamoja na kuongeza wageni wanaotembelea na tokea Oktoba 2023 hadi sasa watalii 239 wametembelea eneo hilo, 52 ni watalii kutoka mataifa ya nje na 187 ni watalii wa ndani.

Alifahamisha kwamba katika muda mfupi huo, tayari 

wamekusanya shilingi za Kitanzania Milioni 11,675,000/=, 

kutoka kwa wageni wanaotembelea eneo hilo ikizingatiwa 

hata msimu wa utalii haujaanza.

“Msimu wa utalii ukifia tunatarajia kuwapokea watalii wengi, 

winge waliofika wamevutiwa na uoto wa asili uliopo, 

Wanyama wengi wanaonekana kwa urahisi kama vile Twiga, Tembo, Pofu, Nyati, pamoja na kupanda mlima kipara kuona uchomojazi na utuaji wa jua,”alisema.

Nae Afisa Uhifadhi na meneja wa Makuyuni Wildlife Park 

uwamangi Andrew Kishe, alisema katika eneo hilo limejaliwa 

kuwa na vivutio mbali mbali vya utalii, mandhari yenye 

kupendeza, sehemu tambarare, maeneo ya miinuko ya 

milima, huku watalii wengi wakivutiwa na kupanda mlima kipara.

Alisema eneo hilo limejaliwa kuwa na kivutio cha 

Wanyamapori aina ya kipekee akiwemo Choroa, 

ikilinganishwa na maeneo mengine ya hifadhi kama vile 

Tarangire, Serengeti, sambamba muonekano wa wanyama 

kwa uzuri, Tembo, Twiga, Makundi makubwa ya Pofu, Nyati na Pundamilia.

Akizungumzia suala la ujangili wa wanyamapori, meneja uyo, 

alisema TAWA imeweka rasilimali watu na vitendea kazi 

katika eneo hilo, kwa kufanya doria za mara kwa mara kwa 

kuzunguka ndani na nje ya mipaka ya eneo kuhakikisha 

majangili hawapati fursa ya kuua wanyamapori.

“Pia tumezuia uingizaji wa mifugo ndani ya eneo hili, imekua 

ni changamoto kubwa kwa jamii iliotuzunguka jamii ya 

Kimasai, kipindi cha kiangazi maeneo yao ya nje 

wanayotegemea kulisha mifugo yao yakikauka hupendelea 

kuingia ndani ya eneo letu, lakini kwa sasa kwa sababu ya 

doria tunazofanya mara kwa mara tatizo hilo limeweza 

kudhibitiwa,”alisema.

Kwa upande wa ukataji wa miti, alisema walilazimika 

kuelimisha jamii kuachana na ukataji wakuni na miti ya 

kujengea nyumba zao, kwani eneo hilo ni kwa faida yao na 

vizazi vyao vinavyokuja, baada ya kuona wanavyonufaika na 

utalii sasa wao wamekua walinzi wakubwa.

Alisema watalii wanapokuja na kuhitaji ngoma za kitamaduni, 

basi jamii ya kimasai inayonzunguka eneo hilo ndio inayotoa 

burudani na kupata fedha kwa ajili ya shughuli zao.

Nae afisa uhifadhi daraja la kwanza na afisa mawaliano ya 

umma na masoko TAWA kanda ya Kaskazini Yuthnes Godfrey 

Nestory, alisema eneo lao ni jipya na lina upekee na uzuri 

ambao haupatikani kwenye hifadhi nyengine zozote Tanzania.

Aliwataka wananchi kutumia nishati mbadala ya kupikia na 

kuachana na matumizi ya kuni na mkaa, kufanya hivyo 

wataweza kupunguza uharibifu wa mazingira kwa ukataji wa 

miti, ikizingatiwa ndio kivutio cha wanyamapori.

Hata hivyo nae Mkurugenzi wa JET JohN Chikomo, 

alilishukuru shirika la USAID kupitia mradi wa Tuhifadhi 

Maliasili unatekelezwa na JET, kwa kufanikisha ziara hiyo 

kwa waandishi wa habari za Mazingira.


BAADHI ya Wanyama pori wanaopatikana kwa wingi katika eneo la Makuyuni Wildlife Park, Twiga, Pundamilia, Tembo, Nyati, pofu, swala, kutokana na uzuru wa mazingira ya eneo hilo la Makuyuni Wildlife Park.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.