Na.Mwandishi OMKR Pemba.
Mwenyekiti wa Chama cha ACT – Taifa
Mhe. Othmani Masoud Othman, amesema kwamba chama hicho kinaamini kwamba Zanzibar inazofursa nyingi za kuweza kupiga hatua za kimaendeleo ya kiuchumi na wananchi kuondokana na umasikini kinachohitajika ni
uongozi wenye maono kama inavyotokea kwa nchi nyengine duniani.
Mhe. Othman Masoud ambaye pia ni Makamu wa
Kwanza wa Rais wa Zanzibar ameyasema hayo huko
Ukumbi wa Dolphini Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba alipokutana na viongozi
wa Chama hicho wa Wilaya za Wete na Micheweni Kichama akiwa katika muendelezo wa
ziara yake ya kukutana na viongozi wa chama hicho ngazi ya mikoa, wilaya na
matawi.
Amesema kwamba viongozi wenye
maono, uwezo wa kujitoa na kujitolea watakoweza kupanga na kutekeleza mikakati
sahihi hya kiuchumi na kimaendelea kutaweza kuisaidia nchi kupiga hatua kwa
kuzitumia fursa na rasilimali za nchi na wananchi kuweza kuongeza kipato
kikubwa na kupambana na umasikini.
Amefahamisha kwamba zipo nchi mbali
mbali duania ambazo zilikuwa na uwezo duni katika kipindi cha miaka ya nyuma
lakini viongozi wake walitumia juhudi , maono na uwezo wako na hivyo kuweza
kuzibadili nchi zao kiuchumi na kimaendeleo jambo amalo linawezekana pia kwa
Zanzibar.
Aidha amesema kwamba katika kufikia
ndoto za namna hiyo viongozi ni lazima
kuwa wa kweli na wenye kuwa na mamlaka na uwezo wa kupanga na kutekeleza
mikakati mbali mbali ya kiuchumi ambayo
itaweza kupambana na hali ya umasikini na kuwasiadia wananchi kuweza kupiga
hatua.
Amesema kwamba hali ilivyo sasa ya
ukali wa maisha kwa wananchi inapelekea kuwepo baadhi ya watu kuwa na fikra na matamshi ya kujutia kuzaliwa
Zanzibar badala ya kujinasibu na uzanzibari wao.
Amewataka wanacnhi kuungana na
chama hicho ambacho kimejimbambanua kwamba kinawajibu , uwezo na malengo ya
kupigania haki za Zanzibar ndani ya muungano jambo ambalo haliwezi kufanywa
na Vyama vyengine.
Alisema kwamba maendeleo ya kweli
ndani ya nchi kamwe hayataletwa kwa ihsani ya mataifa ama mtu yoyote, bali
yatapatikana kutokana na juhudi za kweli kati ya wananchi na viongozi kwa
kutumia rasilimali zao wenyewe.
Akizungunzia suala la serikali ya
Umoja wa Kitaifa amesema kwamba chama chake kinaendelea kutumia hekima baada ya
kufanya mazungunzo na viongozi wakuu lakini tayari kimeshafanya maamuzi ya
kujitoa iwapo mambo ya msingi waliyokubaliana hayatatekelezwa .
Aliyataja masuala hayo kwamba ni
pamoja na kuondoshwa kura ya mapema , kufanyiwa marekebisho mfumo wa uchaguzi
pamoja na sekteratieti ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar pamoja na suala la wananchi
kunyiwa vitambulisho vya uzanzibari Mkaazi.
Kwa upande wake Makamu mwenyekiti
wa Chama hicho Ismail Jussa Ladhu amewaomba viongozi na wananchama wa chama
hicho kutoyasahau malengo na dhamira ya chama chao kwa kufikiria kupata vyeo
vya uwakilishi na ubunge.
Amsefahamisha kwamba masuala hayo
sio lengo la chama na kufanya hivyo kwa njia ya tamaa ni kuleta mgawanyiko
ndani ya chama na kwamba watakaobainika kuendelea na malengo hao chama hakitawaunga
mkono kwa kuwa sio malengo yao.
Amesema masuala yote yanayoleta
mgawanyiko ni kuharibu chama hicho na kwamba ni miongoni mwa masuala ambayo
chama hakiweza kuyapa nafasi kuendelea kufanywa na watu wenye taama na uchu wa
kupata vyema kwa kuwa waasisi wa chama hicho walijitolea na kuacha vyeo vikubwa walivyokuwa navyo kwa
kuzingatia kuweka mbele maslahi ya nchi na kuweka mbele uzalendo.
Mwenyekiti huyo wa ACT- yupo
kisiwani Pemba kukutana na viongozi wa chama hicho ngazi ya matawi , majimbo ,
wilaya na mikoa ikiwa ni hatua ya kutoa shukrani ya kuchaguliwa kwa nafasi hizo katika
uchaguzi mkuu wa chama uliofanyika Mwezi Machi mwaka huu huko mjini Dar es
Salaam.
Mwisho.
Imetolewa na ofisi ya Makamu wa
Kwanza wa Rais wa Zanzibar kupitia kitengo chake cha habari leo Jumanne tarehe
30.04.2024.
No comments:
Post a Comment