Ameyasema hayo wakati wa ufunguzi wa Skuli ya Msingi ya Chanjaani Jombwe Wilaya ya Mkoani, Mkoa wa Kusini Pemba ikiwa ni muendelezo wa shamra shamra za kutimia miaka 61 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.
Amesema kazi kubwa imeshafanywa na Serilikal ya Awamu ya Nane (8) ya kuimarisha miundombinu ya elimu katika kila Wilaya Unguja na Pemba hivyo amewataka wananchi wa Jimbo la Kiwani kuwasimamia na kuwahimiza vijana katika suala zima la kuwapatia elimu ili kuweza kutoa wataalamu wengi na weledi watakaolisaidia na kuliongoza Taifa.
Amewataka wananchi wa Chanjaani Jombwe na maeneo jirani kuthamini maendeleo yanayoletwa na Serikali na Chama Mapinduzi kwa kuiitunza miundombinu inayoendelea kujingwa ndani ya Jimbo lao ili iweze kudumu kwa muda mrefu na kuwanufaisha vizazi vya sasa na vijavyo.
Mhe.Hemed ameuwagiza uongozi wa Wizara ya Elimu kuajiri walimu wazawa na wanaoishi karibu na maeneo yanayojengwa skuli hizo ambao watasaidia kutatua changamoto ya uchelewaji na utoro wa walimu maskulini na kufanikisha azma ya Serikali ya kuondosha Zero kwa skuli za Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais amesema Serikali ipo katika mchakato wa kuzijenga barabara Kuu na Barabara za ndani kwa kiwango cha lami katika Wilaya ya Mkoani jambo litakalorahisha upatikanaji wa huduma ya usafiri, kukuwa kwa uchumi na kuongezeka kwa thamani kwa maeneo yote yatakayopitiwq na Barabara hizo.
Sambamba na hayo Mhe.Hemed amewataka wananchi wa Mwambe na maeneo jirani kuhakikisha wanashirikiana kwa kila hali ili kuhakikisha wanapiga hatua kimaendeleo pamoja na kuimarisha amani na utulivu uliopo kwa maslahi mapana kwa vizazi vya sasa na baadae.
Nae Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Lela Mohamed Mussa amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya elimu imeweka Mifumo mbali mbali ya Elimu katika skuli za Zanzibar inakwenda kuondosha kabisa kiwango cha zero katika mitihani ya kidato cha nne(4) na kidato cha sita(6) na kuongeza kiwango cha ufaulu nchini.
Waziri Lela amesema vifaa vyote pamoja na walimu watakaofundisha skulini hapo wapo tayari na Wizara kwa kushirikiana na Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA) imejipanga kuitatua changamoto ya maji safi na salama kijijini hapo ili wananfunzi, walimu na wananchi waweze kunufaika na huduma hio muhimu kwa maisha ya kila siku ya binaadamu.
Akisoma Taarifa ya Kitaalamu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Ndugu Khamis Abdalla Said amesema Skuli ya Msingi Chanjaani Jombwe iliyojengwa ya ghorofa mbili(G+2) na Mkandarasi Mwinyi Building Construction imejumuisha madarasa 29, maabara, maktaba , ofisi za walimu, chumba cha Kompyuta na kumbi za mikutano hadi kumalizika kwake imegharimu zaidi ya shilingi za Kitanzania Bilioni 4.2.
Katibu Khamis amesema kukamilika kwa ujenzi wa skuli ya Chanjaani Jombwe unakwenda kutatua changamoto ya wanafunzi kufuata skuli maeneo ya mbali panoja ambapo zaidi ya wanafunzi 1300 watapata fursa ya kujisomea katika skuli hio kwa shift ya mkondo mmoja wa asubuhi kwa wastani wa wanafunzi 45 kwa kila darasa.
Amefahamisha kuwa Madarasa yote katika skuli hio yamewekwa samani za kutosha pamoja na vifaa vya kisasa vya kusomea na kufundishia vinavyoendana na Teknoloji ya kisasa jambo litakalosaidia kunyanyua kiwangocha ufaulu ndani ya Mkoa huo.
Imetolewa na Kitengo cha Habari ( OMPR )
Leo tarehe 02 / 01 / 2025..
No comments:
Post a Comment