Habari za Punde

MARAIS WASTAAFU WA ZANZIBAR WAMPONGEZA RAIS DK.MWINYI KWA USHINDI NA KUDUMISHA AMANI .

 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akiwa katika picha ya pamoja na Marais Wastaafu wa Zanzibar (kulia kwa Rais) Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe.Dkt.Amani Abeid Karume na (kushoto kwa Rais) Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe.Dkt.Ali Mohammed Shein.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amekutana na Marais Wastaafu wa Zanzibar, Mhe. Dkt. Ali Mohamed  Shein wa Awamu ya Saba na Mhe. Amani Abeid Karume wa Awamu ya Sita, Ikulu Zanzibar tarehe 08 Novemba 2025.

Marais hao wastaafu wamemtembelea Rais Dkt. Mwinyi kwa lengo la kumpongeza kwa ushindi wa kishindo alioupata, pamoja na kupongeza hali ya amani na utulivu iliyoshuhudiwa wakati wa Uchaguzi Mkuu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.