Joseph Ngilisho, ARUSHA
MGOMBEA Ubunge,katika jimbo la Arumeru Mashariki kupitia CHADEMA, Joshua Nasari amesema usiri wa Wabunge wa kushindwa kufichua na kuweka wazi matumizi ya fedha zinazotolewa kwa ajili ya maendeleo ya mfuko wa jimbo, unachangia umasikini kwenye majimbo.
Alisema Wabunge wengi wamekuwa hawatimizi wajibu wao kwa kushindwa kuwaeleza wananchi usahihi wa matumizi ya fedha hizo na badala yake zimekuwa zikitumika kinyume na makusudio, hali inayowafanya wananchi waendelee kuteseka.
Nassari alibainisha hayo katika kijiji cha Ngurdoto, akiwa kwenye mkutano wa kampeni wa kuomba kura kwenye uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru Mshariki.
Mgombea huyo alisema mara nyingi wananchi hushindwa kutambua fedha za mfuko wa jimbo na kujiuliza zinatolewa kwa ajili gani, hali ambayo kwa sasa imefanya hata baadhi
Alisema endapo atachaguliwa atahakikisha fedha hizo zinatumika kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya wananchi na kwamba hatakuwa Mbunge mbumbumbu na wala hatokuwa Mbunge anayelala na kusinzia akiwa Bungeni.
“Siombi kura kwa ajili ya kwenda kusinzia Bungeni, sitakuwa mbumbumbu nitajitahidi kuhakikisha natetea maslahi ya wananchi kwa wakati wote”,alisema Nasari.
Alisema kwa siku za nyuma katika jimbo
“Kila mwaka zinatolewa milioni 47 kwa ajili ya mfuko wa maendeleo jimbo lakini wananchi hawazioni matumizi yake na kuendelea kubeba changamoto za kijamii, mimi napenda kuwaambia kuwa ni haki yenu ya msingi kuhakikisha kuwa mnajua maana halisi ya mfuko huu wa jimbo”, alisema Nassari.
Alisema kwa sasa jamii zinalia na watoto wa kike kupata ujauzito wakiwa katika masomo na wakiwa katika umri mdogo bila kujua sababu halisi kuwa ni hali ya maisha ambayo wanaishi watoto hao.
“Leo watoto wa kike wakipata mimba watu wanalalamika lakini wanashindwa kujua kuwa endapo
Alifafanua endapo atashika nafasi hiyo ya uongozi katika jimbo hilo, fedha za mfuko wa maendeleo ya jimbo kwa kiwango kikubwa zitatumika kwa ajili ya maendeleo endelevu ya jamii.
No comments:
Post a Comment