Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la
Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,alipokuwa akizungumza na Wajumbe wa
Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Zanzibar,waliofika Ikulu Mjini
Zanzibar leo.[Picha na Ramadhan Othman.Ikulu.]
 Na   Idara ya  H/Maelezo 
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mh. Dk Ali Mohammed Shein anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi  Duniani May  Day  huko Bwawani Mjini Zanzibar 
Kwa mujibu wa  taarifa iliyotolewa naWizara ya Kazi, Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi kupitia kamisheni ya kazi imeeleza kwamba  Sherehe hizo zitaanza  saa  mbili asubuhi kwa maandamano maalum ya Wafanyakazi kutoka Taasisi  mbali mbali za sekta za Ummma na Binafsi.
 Baada ya mapokezi hayo Rais wa Zanzibar anatarajiwa kuzungumza na Wafanyakazi wa Zaznibar na baadae kukabidhi zawadi kwa wafanyakazi  bora kutoka tasisi mbali mbali.
Mapema  Mwakilishi wa Shirika la Kazi Duniani  (ILO) atatoa salam zake kwa wafanyakazi wa Zanzibar ikifuatiwa na risala ya wafanyakazi.. 
 Mapema   waandaaji wa wamaadhimisho hayo ya Siku ya Wafanyaklazi Duniani (MEI DAY) ambao ni Wizara ya Kazi Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi ikishirikiana na Shirikisho la Vyama  Huru vya Wafanyakazi  (ZATUC)  watafanya  usafi wa mazingira  kuanzia tarehe 27 hadi 30 mwezi  huu   katika maeneo ya  Hospitali ya Mnazi Mmoja.,Nyumba za Wazee Sebleni ,Hospitali ya Wagonjwa wa Akili na Afisi za ZATUC Kikwajuni.kuanzia saa 1.00 asubuhi kwa siku zote hizo.
 Aidha taarifa hiyo imeviomba vyombo  vya Habari  kutoa ushrikiano wao katika  kushiriki kikamilifu  kwenya  Sherehe hizo na kuwapa taarifa wanahi wa Tanzania juu ya siku hiyo muhimu. 
Siku ya Wafanya kazi Duniani  hufanyika kila tarehe 1 Mei  Ulimwenguni kote

No comments:
Post a Comment