Na
Abdi Shamnah
WASANII
wa kikundi cha Taarabu cha Tausi, wametakiwa kujituma na kulitangaza vyema jina
la Zanzibar wawapo nje ya mipaka ya
nchi.
Changamoto
hiyo imetolewa leo katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Zanzibar na Naibu
Waziri wa Habari,Utamaduni,Utalii an Michezo, Bihindi Hamad Khamis, wakati
alipowaaga wasanii hao wanaoeelekea nchi za Lebanon na Misri, kushiriki katika Tamasha la
muziki ‘Spring Festival’ litakalodumu kwa muda wa siku tano.
Jumla
ya wasanii 11 wa kikundi cha taarabu cha Tausi, kinachoundwa na akinamama
watupu wanashiriki katika tamasha hilo, chini ya ufadhili wa vituo vya vya
sanaa vya SHAMS ya Beirut na Moreld cha nchini Misri.
Bihindi
alisema Serikali ya Zanzibar ina fahari kubwa kuwa na kikundi cha taarabu cha akinamama
watupu, kinachopiga muziki katika kiwango cha juu, kiasi cha kupata mialiko
kutoka nchi zinazotajika na waanzilishi za muziki huo.
Aliwataka
wasanii hao kudumisha nidhamu katika kipindi chote wawapo ughaibuni.
Hii
ni mara ya kwanza kwa kikundi hicho kupata mualiko wa kuzitembelea nchi za
Mashariki ya Kati, wakati ambapo mwaka 2010 ilipata mwaliko wa kushiriki katika
ufunguzi wa mkutano wa AU mjini
Nairobi,Kenya.
Katika
tamasha hilo nchi mbali mbali kutoka Bara la ulaya , Mashariki ya Kati na Afrika
zinashiriki katika tamasha hilo, zikiwemo Uingereza,Uholanzi,Ujerumani,
Tajikistan,Syria,Iran, Misri na Lebanon.
Wasanii walioondoka kwa safari hio ni pamoja
na Mariam Hamdan (kiongozi wa msafara), Mohammed Ilyas, Sheria Issa, Asha
Khatibu, Topsy Surrie, Wahida Mohammed, Mwaka Mshindo, Tabu Makame, Tatu
Khamis, Fatma Bakar na Fatma bint Baraka ‘Bikidude’.
No comments:
Post a Comment