Habari za Punde

Bajeti SMZ yapita


Amani nguzo ya kukuza uchumi
Tume itumike kuondosha kero ya Muungano

Na Ramadhan Makame

WAJUMBE wa Baraza la Wawakilishi jana wamepitisha makadirio ya bajeti ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mwaka 2012/2013, iliyowasilishwa wiki iliyopita na waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha Uchumi na Mipango ya Maendeleo, Omar Yussuf Mzee.

Wajumbe hao waliipitisha bajeti hiyo, baada ya kazi kubwa iliyofanywa na waziri huyo ya kupokea michangio na kujibu hoja mbali mbali za wajumbe wa Baraza hilo.

Hata hivyo haikuwa kazi rahisi kwani wakati Baraza hilo likikaa kama kamati ya kupitisha mafungu ya matumizi wajumbe hao walilazimika kusimama mara kadhaa kupiga buti wakitaka ufafanuzi wa hoja walizochangia.
  

Awali kabla ya kupitishwa kwa bajeti hiyo wajumbe hao waliwaomba wananchi wa Zanzibar kuhakikisha wanadumisha amani hali itakayohakikisha inastawisha uchumi wa Zanzibar.

Akichangia waziri wa Biashara na Viwanda ambaye pia ni Mwakilishi wa jimbo la Mtoni (CUF), Nassor Ahmed Mazrui, alisema kama Wazanzibari wataendelea kuichafua amali iliyopo uchumi wa Zanzibar utakuwa katika matatizo.

Alisema kwa kiasi kikubwa uchumi wa Zanzibar unategemea utalii na biashara, sekta ambazo haziwezi kuhimili vurugu na kwamba kama yapo malalamiko dhidi ya Muungano yawasilishwe kwenye Tume ya mchakato wa katiba mpya.

Naye Mwakilishi wa jimbo la Magomeni (CCM), Salmin Awadh Salmin, alisema kama Wazanzibari wanataka waendelee kupiga hatua mbele za kiuchumi lazima wahakikishe amani iliyopo inadumu bila ya kuchezewa.
“Tunajua kama matatizo ya Muungano yapo, na yapo kwa muda mrefu, tutumie fursa ya kusema tunachokitaka na tusichokitaka”, alisema Mwakilishi huyo.

Kwa upande wake Waziri Asiye na wizara Maalum, Haji Faki Shaali, alisema Tume ya katiba chini ya Mwenyekiti wake Jaji Warioba, amesema atapokea maoni hata ya wale wasiotaka Muungano.
“Kwa fursa hii iliyopo watakaodhamiria kuvunja amani wana ajenda ya siri, kwanini wasitumie nafasi hii kueleza yanayowasibu”,alisema waziri huyo.

Naye waziri wa Kazi Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika, Haroun Ali Suleiman, aliwataka wananchi watumie fursa ya Tume kutoa maoni na asiwepo mtu wa kuzuiwa kutoa maoni yake juu ya Muungano.

 Katika michangio yao ya jumla wajumbe hao waliishauri serikali kuhakikisha inatilia mkazo utekelezwaji wa Mapinduzi ya kilimo, ambapo ni miongoni mwa sekta zilizopewa kipaumbele katika bajeti hiyo.

Mbarouk Wadi Mussa (Mtando)

Mipango mizuri inabuniwa lakini tatizo lipo katika utekelezaji hali inayochangia wananchi kushindwa kupata matunda ya mipango hiyo.

Serikali imepunguza pembejeo za kilimo lakini wananchi wengi hawakunufaika nalo kutokana na mpango wa kilimo utekelezaji wake kuwa mabaya.

Kwanini serikali inapata kigugumizi kueleza utekelezaji wa mapendekeo ya kamati teule imebainisha upotevu mkubwa wa fedha za umma.

“Serikali itueleze maana yale wananchi wanayajua sasa kwanini serikali inapata ugumu wa kueleza.

Mpango wa kukusanya mapato bado uko lege lege, serikali haijawa tayari katika suala la ukusanyaji wa kodi mianya ya kodi ipo mingi serikali ioneshe nia thabiti bado kunaudhaifu.

Sekta ya utalii bado kodi zake hazijainufaisha sana serikali wawekezaji wa kigeni wanapewa misamaha

Waziri aeleze kwanini kodi ya wafanyakazi wa serikali ya Jamhuri walipo Zanzibar imeshindwa kukusanywa.

Serikali imefanya jambo la maana kuweka kipaumbele sekta ya afya, akina mama wanaokwenda kujifungua wasisumbuliwe.

Upo uuzwaji holela wa majengo ya serikali, utaratibu uandaliwe uuzwaji wa majengo ya serikali uhusishe baraza la wawakilishi japo kupitia kamati.

Bikame - ukuaji wa uchumi unatia mashaka kwani hauoneshi kusaidia maisha ya wananchi.

Kipaumbele cha kilimo serikali haikujipanga kumejitokeza changamoto kadhaa ikiwemo kutopatikana kwa wakati pembejeo za kilimo. Mapinduzi ya kilimo yatafikiwa endapo mipango itatekelezwa.

Serikali ijipange kama inataka kuhakikisha inatekeleza mapinduzi ya kilimo.
Udhibii wa Mfuko wa bei uangaliwe unawaathiri wananchi kimaisha.
Rais apongezwa kwa kuondoshwa ada ya akina mama wajawazito, maandalizi yaandaliwe ili mizwengwe iondoshwe kwenye  

Salmin Awadh Salmin (Magomeni) – 

Serikali inakusanya fedha katika taasisi zake kwa makadirio. Kodi zisikusanywe kwa makadirio dunia imeondokana na njia hiyo ya ukusanyaji wa kodi.
Utaratibu huo wa makadirio ndio unaosababisha wa kudokolewa kwa mapato.
Kipaumbele cha huduma ya afya,

Haji Faki Shaali - ada ya bandari ya shilingi 1000 iliyoongezwa itatumika kunufaisha watoto wa kizanzibari kwa kununuliwa madawati ya kukalia skuli.

Bajeti ya mwaka huu ni nzuri kwani matumizi fungu la maendeleo ni kubwa kuliko fungu la matumizi ya kawaida. Hali hiyo itaifanya nchi kupiga hatua.
Atakayefanya vurugu atakuwa na ajenda ya siri kwani jaji Warioba amesema atapokea hadi maoni ya wasiopenda muungano.

Wananchi waungane kueleza yale yanayowakera katika kero za muungano.
Wazanzibari watafute vitu vitakavyowaunganisha katika utoaji wa maoni ya katiba na kusahau tofauti za kisiasa na kidini.

 Nassor Ahmed Mazrui

Kukua kwa pato la 6.8 ni hatua kubwa utalii, biashara vimeimarika bidhaa kutoka Z’bar kwenda bara 2011 urari wa biashara kati ya T bara na Z’bar umekuwa 71.39     bilioni 74.73  urari 2010 tofauti ilikuwa zaidi ya bilioni 21     
Karafuu nazo zimesaidia seka ya bishara imekuwa mara tatu kutoka asilimia saba hadi 21, mipango iliyopo ni kukuza aidi ya bishara
Utalii umekuwa mara tatu zaidi

Serikali haikulala juu ya suala la kuimarisha viwanda, kazi inafanyika kuhakikisha mazingira mazuri yanawekwa kuvutia wawekezaji watakaoweka viwanda.

Zanzibar inakabiliwa na changamoto nyingi kwa wawekezaji wa viwanda ikiwa ni pamoja na bandari na umeme.

Suala la kukua kwa biashara visiwani Zanzibar linategemea amani na utulivu, amani ni nyenzo ya kujenga uchumi imara. Hakuna mtu atakayekuja kujenga nchi hii.

Katiba tuitakayo itapatikana kwa wananchi kujitokeza kutoa maoni umoja mshikamano kwa Wazanzibari unahitajika katika muda huu kuliko muda wowote.



4 comments:

  1. Kupita kwa bajeti nlikutarajia, wawakilishi wenyewe alina Omar Ali Shehe?..unatarajia nini hapo?

    ReplyDelete
  2. Ni ajabu na kweli pale unapoona bajeti ikielekeza namna ya kujikwamua kutonana na utegemezi lakini wawakilishi wetu ndiyo vinara wa kukatisha jitihada hizo za kuondokana na utegemezi. Tozo ya kdi ya bandari kwa abiria kwenda Pemba ilikuwa sahihi kabisa kwa hivle wananchi watachangia upatikanaji wa madawati kwa ajili ya watoto wao kutoka kwenye nguvu za wananchi wenyewe. Lakini sasa itabidi madawati hayo yasinunuliwe na watoto waendelee kukaa chini wakati wawakilishi wakinesa kwenye viti barazani huku wakipata upepo mwanana wa air conditioners...

    ReplyDelete
  3. W'bari walimuelewa vibaya MZEE KARUME, pale alipoamua baadhi ya huduma za jamii ziwe bure, kwa vile ilikua ndio kwanza tunapata uhuru na hivyo wananchi walikua hawajajipanga.

    Leo hii miaka takriban 50 tokea tupate uhuru lkn watu bado kila kitu wanataka kiwe bure, inapendeza lkn uwezo uko wapi?

    Kweli Wazeji ni masikini lkn mambo mengine hayahitaji utajiri ni suala la kipaombele tu, hivi inakuaje mtu anaelalamikia umaskini lkn ana wake watatu au wanne?

    Wakati umefika kwa SMZ kuacha kuongoza nchi kwa hisia, kama huduma inahitaji kuchangiwa serikali itoze mchango mara moja!

    Mimi naamini kama SMZ itakua makini ktk kuchangisha baadhi ya huduma Wanachi nao watakua makini ktk kupanga familia. Hivi inakuaje mtu awena wake 4 na watoto 12 ategemee serikali kumsomeshea na kumtibia bure yeye anachangia nini serikalini? Aidha huduma za matibabu maalum kama vile KANSA, FIGO,INI, MOYO nk. serikali inatakiwa kutoa huduma hizi kwa malipo ili waweze kumudu kiziendesha na hivyo kuwapunguzia watu gharama zaidi za kwenda kutafuta huduma hizi idia, afrika kusini na Bara.

    Najua wadau hawata nielewa lakini huu ndio ukweli Dunia nzima inafanya hivyo hatuwezi kua tofauti!...sasahivi karibia huduma zote za serikali zina suasua!

    ReplyDelete
  4. Ukitaka kuipata pepo lazima ufe...na tukitaka kupata madawati maskulini ni lazima tuchangie. Uhaba wa vifaa vya kufundishia na hata tiba vinatokana na wananchi kutochangia na kuwekwa vipaumbele. Tumepoteza nafasi muhimu sana ya kujikwamua kutokana na utegemezi wa misaada.

    Sioni sababu kwa wawakilishi kuwa katika kampeni zisizokwisha.

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.