Joseph Ngilisho, Arusha
CHAMA cha Demokrasia na
maendeleo (Chadema) kimetoa onyo kali kwa baadhi ya madiwani wake jijini Arusha
walioshiriki katika mchakato wa maandalizi ya uzinduzi wa jiji la Arusha
kinyume na msimamo wa chama hicho.
Pia,chama hicho juzi kiliwaweka
kiti moto madiwani hao na kuwahoji kuhusu tuhuma za kushiriki vikao vya Baraza
la madiwani la jiji hilo sanjari na kuchukua posho mbalimbali za vikao hivo
ambapo walijieleza na maelezo yao kufikishwa katika ngazi za juu.
Akizungumza na waandishi wa
habari jijini Arusha, katibu mkuu wa Chadema ,Dk Willbrod Slaa alisema kuwa
iwapo itabainika baadhi ya madiwani hao walijipenyeza na kushiriki mchakato wa
uzinduzi wa jiji hilo pamoja na kuchukua posho za vikao mbalimbali wataadhibiwa
kwa mujibu wa taratibu za chama hicho.
Dk, Slaa alisema kuwa msimamo
wa chama hicho ni kutomtambua meya wa Arusha ,Gaudence Lyimo(ccm)kwa kile
alichodai taratibu za kupatikana kwake hazikufuatwa,na kusisitiza kuwa iwapo
madiwani wake wanajipenyeza na kushiriki vikao vya halmashauri vinavyoongozwa
na meya huyo ni utovu wa nidhamu.
‘’kitendo cha kushiriki vikao
vya halimashauri ni kuhalalisha kumtambua meya wa Arusha sasa sisi msimamo wetu
ni kutoshiriki vikao na hata madiwani wanalijua hilo ila kama wanashiriki
kinyemela na kuchukua posho tutapambana nao’’alisema Dk Slaa.
Aidha dkt Slaa alionya kuwa
kitendo cha madiwani wake kushiriki vikao vya manispaa ni mwanzo mbaya wa
kuambikizwa madhambi ya ufisadi yaliyopo ndani ya manispaa hiyo ukiwemo
matumizi mabaya ya fedha za wananchi.
Hata hivyo mwandishi alipotaka
kujua msimamo wa Chadema utaisha lini wakati wananchi wanaendelea kusota kwa
kukosa wawakilishi kwenye kata zao,alisema kuwa diwani anapaswa kushiriki
maendeleo kwenye kata yake na wananchi wake na si kushiriki vikao vya
halmashauri.
Aliongeza kuwa diwani anapaswa kumfuata ofisini mkurugenzi wa jiji na kumweleza matatizo yaliyopo kwenye kata yake bila kushiriki vikao vya baraza la madiwani.
Alipotafutwa mwenyekiti wa
madiwani wa Chadema jijini hapa,Isaya Doita ambaye ni diwani wa kata ya
Ngarenaro alikiri hatua ya wao kuhojiwa na Dk Slaa huku akisema kwamba kwa sasa
hawana la kusema kwa kuwa wanasubiri maelekezo kutoka ngazi za juu za chama.
Hatahivyo,alikiri wao kushiriki
mchakato wa uzinduzi wa jiji la Arusha hivi karibuni huku akidai ya kwamba
suala la kushiriki na kupokea posho za vikao mbalimbali ni halali yao.
Itakumbukwa ya kwamba onyo
lililotolewa na Dk Slaa limekuja siku chache baada ya madiwani wa CCM,Tlp na
Chadema jijini Arusha kushiriki mchakato wa uzinduzi wa jiji hilo kitendo
ambacho kimeibua gumzo jijini hapa huku ikikumbukwa ya kwamba madiwani wa
Chadema waliweka msimamo wa kutomtatabua meya wa jiji la Arusha.
Baadhi ya madiwani wa Chadema
walioshiriki mchakato wa uzinduzi wa jiji hilo hivi karibuni waliongozwa na
diwani wa kata ya Levolosi,Efatha Nanyaro ambapo alichaguliwa kuwa katibu wa
maandalizi ya chakula cha Rais huku mwenyekiti wake akiwa ni diwani wa kata ya
Moshono,Paul Matyhsen(CCM).
Vilevile itakumbukwa ya kwamba
Chadema kiliwahi kuwatimua madiwani wake watano mwaka jana ambao ni John
Bayo,Ruben Ngowi,Estomi Malah na Rehema Mohamed kwa kosa kuingia mwafaka wa
kumtabua meya wa jiji la Arusha.
No comments:
Post a Comment