Na Masanja Mabula,Pemba
WATU
13 wamenusurika kufa kufuatia ajali ya gari ya kampuni ya HYOUNG inayojenga
barabara tano katika mkoa wa kaskazini Pemba
kuacha njia na kupinduka katika eneo la Tumgamaa wilaya ya Wete.
Kamanda
wa Polisi wa Mkoa wa Kaskazini Pemba , Kamishna Msaidizi Mwandamizi Yahya
Rashid Bugi alisema tukio hilo limetokea jana
majira ta saa 12:45 asubuhi wakati gari hilo
lilipokuwa limechukua wafanyakazi wa ujenzi wa barabara kuwapeleka Mtambwe
kuendelea na kazi za ujenzi.
Alisema
ajali hiyo imelihuisha gari lenye namba za usajili Z518 BK ambalo lilikuwa
linaendeshwa na Hassan Mohammed mkaazi wa Pandani ambaye ni miongoni wa
majeruhi waliolazwa katika hospitali ya Wete.
Kamanda
Bugi amesema chanzo cha ajali hiyo ni baada ya gari hilo kugoma breki wakati dereva akiwa anataka kubadilisha gia
alipokuwa akipandisha mlima na hivyo gari kuacha njia na kuangukia bondeni.
"Licha
ya kwamba uchunguzi wa ajali hiyo bado unaendelea, lakini taarifa ambazo tunazo
ni kuwa gari hilo liliacha njia na kuanguka baada ya gia kugoma, na dereva
kushindwa kulidhibiti na kusababisha kuangukia bondeni," alifahamisha
Bugi.
Naye
Mkuu wa wauguzi katika hospitali ya Wete,
Dk. Seif Said amesema wamepokea majeruhi 11 wa ajali hiyo na kwamba baadhi yao hali zao ni mbaya.
Aliwataja
majeruhi waliofikishwa katika hospitali hiyo kuwa ni Salma Abdullah Ali
aliyepata maumivu katika sehemu za kiuno , mgongo na sehemu za shingoni na Fatma Juma Said , ambaye ameumia kwa
kuvunjika mkono na mguu pamoja na sehemu za usoni.
Wengine
ni Fadhila Rashid Mbarouk , Abdillah Hamad Baucha , Said Ubwa Daudi , Joseph
Owino, Madila S Soud , Abdalla Mohemmed
Said , Andros Wakenya pamoja na mtoto mwenye umri wa miaka 6 Abdi Juma Machano
aliyeumia kwa kuvunjika mkono.
Kufuatia
ajali hiyo,Kamanda Bugi amewataka madereva kuzingatia sheria za usalama
barabarani ili kuweza kuzuia kutokea ajali zisizokuwa za lazima.
Hii
ni ajali ya pili kutokea katika Mkoa wa Kaskazini Pemba katika kipindi hichi
cha mwezi Januari ambapo wiki iliyopita ajali iliyotokea katika wilaya ya
Micheweni ilisababisha kifo cha mtu mmoja na wengine kujeruhiwa.
No comments:
Post a Comment