Joseph Ngilisho,Arusha
TANZANIA
bado inakabiliwa na idadi kubwa ya akina mama wajawazito, wanaojifungulia
majumbani, ambapo hadi kufikia mwaka 2012 asilimia hamsini ya wajawazito nchini
hujifungulia majumbani, licha ya jitihada za serikali zinazofanywa.
Hayo
yalisemwa jana na Waziri wa Afya na Ustawi wa jamii, Dk. Hussein Mwinyi, wakati
akimkaribisha Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal,
kwenye
mkutano wa unaozungumzia uboreshaji na maendeleo ya mama na mtoto, unaofanyika
jijini Arusha na kuwashirikisha wajumbe zaidi ya 800
kutoka
nchi 68 duniani.
Alisema
serikali imeweka mikakati mbalimbali ya kukabiliana na vifo vya akinamama na
watoto, ikiwa pamoja na utoaji wa huduma ya kujifungua na vifaa vyake bure,
lakini bado akina mama wanakwepa
kwenda
hospitali na vituo vya afya kujifungua.
Dk.
Mwinyi alisema zipo sababu nyingi zinazosababisha vifo hivyo, lakini pia kubwa
linachangiwa na mimba za utotoni chini ya miaka 18 ambapo sasa serikali
inajikita kuelimisha wanafunzi na wazazi madhara ya kubeba mimba katika umri
mdogo.
“Lakini
pia tunataka ifikapo mwaka 2015 angalau kila kijiji kiwe na kituo cha afya na
kila Kata iwe na zahanati, ili kusogeza huduma ya kujifungulia karibu na
jamii,” alisema.
Dk.
Mwinyi alisisitiza umuhimu wa mpango wa kila familia, katika kuhakikisha afya
ya mama na mtoto inalindwa.
Alisema
ili kukabiliana na changamoto mbalimbali za sekta ya afya,serikali imetoa fedha
nyingi katika kuhakikisha vijana 7,000,wanasoma katika vyuo vya afya, kila
mwaka na wanapohitimu serikali
inahakikisha
inawaajiri katika hospitali na zahanati za serikali ili kupunguza tatizo hilo.
Naye
Makamu wa Rais Tanzania,
Dk. Mohammed Gharib Bilal, akifungua
mkutano huo alisema licha ya Tanzania
kukimbizana katika kutimiza malengo ya
milenia,
lakini bado tatizo la vifo vya watoto ni kubwa, ambapo kila penye watoto 20,
mtoto mmoja hufa hali ambayo inapaswa kutiliwa mkazo kuondoa hilo.
“Hii
takwimu siyo nzuri na inatisha kuona watoto hawa wanapoteza maisha, wakati upo
uwezekano wa kulimaliza hili na kuokoa maisha ya watoto wetu,” alisema.
Alisema
kwa Tanzania tatizo la vifo vya akinamama ni kubwa, lakini limepunguzwa kutoka
770 mwaka 1990 hadi 454 mwaka 2010 kati ya akinamama 100,000 wanaofika
hospitalini kujifungua.
Alisema
vifo vya kinamama na watoto, vinazidi kuongezeka haswa katika nchi
zilizoendelea, lakini kwa upande wa Tanzania inahakikisha hakuna
mtoto
wala mama atakayekufa, kutokana na matatizo ya uzazi ifikapo 2015.
Pia alitoa rai kwa watalaamu wa afya duniani,
kuendelea kufanya tafiti za vyanzo vya vifo hivyo na kuzitoa, huku
wakihakikisha zinafanyiwa kazi.
Kwa upande wake Waziri wa afya, kutoka nchini
Rwanda, Dk. Agnes Binangwaho alisema Rwanda, inafanikiwa kupunguza vifo vya
mama na mtoto, kutokana na kutoa elimu kwa wananchi juu ya uzazi wa mpango,
pamoja na kusambaza simu kwa kila muuguzi wa kituo cha afya na kutoa namba kwa
wananchi ili wakiwa na matatizo gari la wagonjwa huwafuata mahali walipo na
kuwakimbiza hospitali, kupata huduma mbalimbali ikiwemo kujifungua.
unyanyasaji na mateso yamekithiri kutoka kwa manesi na madaktari , nani atakwenda kujifungua hospitali? matusi ya nguoni , kufinywa na kupigwa wakati mwengine au kubwanwa na mikasi huku unapewa matusi mazito mazito , unajuta kubeba mimba.....aaah jamani.... sijui niseme nini .. tena hao wazalishaji wengi ni wanawake ambao nao uchungu wanaojua lakini madhila wanayotufanyia sina maneno....
ReplyDelete