Na
Kunze Mswanyama,DSM
UTARATIBU
wa upimaji wa mabasi na malori ya mizigo katika mizani mbalimbali
nchini,umetajwa kuwa chanzo kitakachoichelewesha Tanzania kufikia maendeleo ya
haraka mara baada ya soko la pamoja la biashara kwa nchi za Afrika Mashariki
litakapoanza.
Kauli
hiyo imetolewa juzi jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Msafara wa Wanafunzi kutoka
Chuo Kikuu cha Kampala (KIU), Shakur Wahad, alipokuwa akizungumza na waandishi
wa habari juu ya matatizo waliyokutana
nayo katika mizani wakati wakiingia
nchini kushiriki michezo ya vyuo vikuu vya Afrika Mashariki na Kati, inayoendelea
katika chuo kikuu cha Dar es Salaam
Akizungumzia
kuhusu matatizo hayo,Wahad alisema anashangazwa na utaratibu huo wa upimaji wa
magari katika mizani tofauti na nchi nyingine za Afrika Mashariki, huku
wakilalamikia kutozwa kiasi cha zaidi ya
shilingi milioni 3 kama faini baada ya
basi lao mali ya chuo hicho walililokuwa wakisafiria kuonekana kuzidi uzito zaidi ya viwango
vilivyowekwa na Wakala wa Barabra nchini (Tanroads).
“Kama
Tanzania itataka kufika mahali ikajivunia kimaendeleo inapaswa kulitazama eneo
hilo, tumetoka Uganda, tumepita Kenya hatujakutana na kikwazo chochote hadi
tulipoingia Namanga kwa upande wa Tanzania ndipo balaa lilipoanza, hii ni
kikwazo kwa maendeleo ya Tanzania ikizingatiwa kuna mipango ya kuingia katika
soko la pamoja,” alisema.
Alisema
walipofika katika mizani ya Namanga,
basi lao lilitozwa faini kwa kuzidisha uzito, na baadae tatizo kama hilo
liliwakuta tena walipofika mizani iliyopo njia panda ya Himo mkoani Kilimanjaro na kisha
katika mizani ya Mkata iliyopo mkoani Pwani.
Aidha
alisema matatizo hayo waliyokutana nayo, yanatokana na wao kutofahamu juu ya
uwepo wa utaratibu wa upimaji katika mizani jambo lililowafanya waamini kuwa
safari yao
ilikuwa salama pasipo tatizo lolote hususani linalohusiana na masuala ya
matumizi sahihi na sheria za barabara.
Wahad
alisema anaamini Tanzania ina fursa
nyingi za kimaendeleo na kwamba ili iweze kujihakikishia inatimiza ndoto zake
kuendelea kukua kiuchumi, ni vyema ikatazama maeneo muhimu yanayochangia kukua kwa uchumi huo ikiwemo njia ya usafirishaji
hasa barabara.
Alipoulizwa
kuhusiana na suala hilo, Msemaji wa Wizara ya Ujenzi, Martin Ntemo, alisema wizara
inalifuatilia suala hilo
ili kufahamu undani wa tatizo walilokutana nalo wanafunzi hao katika mizani na
kisha atalitolea ufafanuzi baadae.
“Kiasi fulani nimesikia taarifa kuhusiana na
suala hilo, lakini naomba nipe muda ili niweze kulifuatilia kwa ajili ya kupata
taarifa kamili halafu nitakujulisha kila kitu juu ya kilichokuwa kimetokea,”
alisema.
Akizungumzia
kuhusu utaribu wa upimaji mabasi katika mizani, Katibu wa Chama cha Wamiliki wa
Mabasi Tanzania(TABOA) Enea Mrutu, alisema Tanzania
inapaswa kujifunza kutoka katika nchi zingine kama
kweli ina nia ya kuboresha sekta ya usafiri.
Alisema
inashangaza kuona utaratibu huo kuwepo Tanzania
pekee suala alilosema ni vyema kama
litatazamwa upya kwa lengo la kuondoa
dosari zilizopo.
No comments:
Post a Comment