Habari za Punde

Washindi wa ‘Kwangua na Ushinde’ wakabidhiwa zawadi zao

 Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel, Zanzibar-Mohamed Mussa akimkabidhi zawadi ya Huawei Media pad mmoja wa washindi wa promosheni ya 'Kwangua na Ushinde', bwana Rashid George Rashid.
Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel, Zanzibar-Mohamed Mussa akimkabidhi zawadi ya Modem ya 3G mmoja wa washindi wa promosheni ya 'Kwangua na Ushinde', bwana Simai Jarabu Idd


Washindi wa awamu ya kwanza wa promosheni ya ‘Kwangua na Ushinde’ ya Zantel iliyozinduliwa wiki iliyopita, wamekabidhiwa zawadi zao leo katika kituo cha Huduma kwa wateja cha Zantel kilichopo Mlandege, Zanzibar.

Washindi waliokabidhiwa zawadi zao leo ni Bi Mwanamvua Suleiman aliyejishindia muda wa maongezi wenye thamani ya shilingi milioni moja, Rashid George aliyejishindia komputa ndogo ya Huawei pamoja na washindi wengine watano wa 3G modem, Simai Iddi, Abdallah Juma, Subira Sheha, Zahor Mzee and Zainab Ali Machano.

Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi hizo, Mkurugenzi wa Biashara wa Zantel upande wa Zanzibar, Mohamed Mussa alisema zawadi hizo ni shukrani ya kampuni ya Zantel kwa wateja wake zikiwa na lengo la kuwasaidia kiuchumi.

‘Zawadi hizi kwa wateja wetu zinadhihirisha nia ya kamupuni yetu ya kuwawezesha wateja wetu kimaisha huku zikiwarahishia mawasiliano na ndugu na jamaa zao’ alisema Mussa.

Promosheni ya ‘Kwangua na Ushinde’ ilizinduliwa wiki iliyopita na mshindi mkubwa atajinyakulia zawadi ya gari huku washindi wengine wakijishindia pikipiki, komputa ndogo za Huawei, modemu za 3G pamoja na muda wa maongezi wa shilingi milioni moja.

Ili kushiriki katika promosheni hiyo wateja wa kampuni hiyo wanapaswa kuweka muda wa maongezi wa shilingi elfu moja au zaidi.

 

Naye Mkurugenzi Mkuu wa kampuni hiyo, Pratap Ghose amewapongeza wateja walioshinda zawadi hizo na kuwasihi waendelee kutumia huduma za Zantel.

‘Kampuni yetu ina dhamira kubwa ya kufanya huduma ya mawasiliano inakuwa nafuu zaidi hapa nchini, na hiyo ni pamoja na kuboresha maisha ya wateja wetu’ alisisitiza Pratap.

 

 

 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.