Habari za Punde

Balozi Seif Akiendelea na Ziara yake Seattle Washington USA.

Balozi Seif akiagana na Naibu Mkurugenzi wa Mfuko wa Kimataifa wa Misaada wa Bill na Melinda Gates Bibi Arlene Mitchell mara baada yha mazungumzo yao katika Ofisi ya Mfuko huo zilizopo kati kati ya Jiji la Seattle.
Kati kati yao ni Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko Mh. Nassor Ahmed Mazrui.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiangalia kifaa kipya kabisa cha mawasiliano ya kompyuta Maarufu ipad kwenye kampuni ya Microsoft akishuhudiwa na Waziri wa Biashara Kushoto yake Mh. Nassor Ahmed Mazrui. Kulia yake ni Mtaa lamu wa Kompyuta wa Kampuni ya Maicrosoft Mhandisi Daniel Moloznk na Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman Iddi.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kati kati akibadilishana mawazo na Mawaziri wake aliofuatanao nao katika ziara yao Nchini Marekani.  Kushoto yake ni Mh. Nassor Ahmed Mazrui Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko  na kulia yake Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mohammed Aboud Mohammed.
Makamu wa Pili wa Rais wa Znzibar Balozi Seif na Ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kutembelea ofisi ya Kampuni ya Microsoft kati kati ya Mji wa Seattle – Washing Nchini Marekani.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif na ujumbe wake akiangalia baadhi ya kompyuta mpya zilizoingia kwenye soko katika ofisi za Kampuni ya Kimataifa bya Microsoft Mjini Seattle – Washington Nchini Marekani.
Balozi Seif akiwa katika picha ya pamoja na Uongozi wa Mfuko wa Kimataifa wa misaada wa Bill na Melinda Gates pamoja na ujumbe aliofuatana nao mara baada ya mazungumzo yao kwenye ofisi ya Mfuko huo Mjini Seattle
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Bingwa wa zamani wa  Mbio za Magari Duniani Robert Shumake aliyekuwa tayari kuingia ubia na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar { ZSSF } katika mpango wake wa ujenzi wa nyumba za mkopo nafuu Mbweni,Robert  Shumake ni Ofisa Mkuu wa Taasisi ya Mtandao wa ushirikiano ya Latin America iliyoanzishwa kwa lengo la kusaidia huduma za Kijamii kama Ujenzi wa Nyumba, Afya pamoja na Elimu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiwa katika picha ya Pamoja na Bingwa wa zamani wa  Mbio za Magari Duniani Robert Shumake kushoto yake  mara baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika katika Hoteli ya Kimataifa ya Marriott Mjini Seattle – Washington Nchini 
Rais wa Chama cha Wafanyabiashara, wenye Viwanda na Wakulima Zanzibar Bw. Abdulla Abass akimpatia zawadi Maalum za Zanzibar Mkurugenzi Mkuu wa kitengo cha Elimu ya Afya cha Microsoft Bwana Bill Crounse Mjini Seattle.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.