Na Mwandishi wetu
SHIRIKA la Umeme Zanzibar (ZECO) litapandisha tena bei ya umeme baada
ya Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) kuliruhusu Shirika
la Umeme Tanzania (TANESCO) kuongeza bei ya umeme.
Akizungumza na kituo cha redio cha Zenj FM jana, Meneja wa Shirika la
Umeme Zanzibar, Nd. Hassan Ali Mbarouk, alisema taratibu za kuongeza bei ya
umeme zinafanywa, ingawa alisema bado hajafahamu malipo hayo mapya yataanza lini.
Alisema kwa sasa wateja wa Shirika hilo wataendelea kulipa bei ya sasa
wakati shirika likiendelea na utaratibu wa kuweka bei mpya.
Bei hiyo mpya inakuja wakati ni hivi karibuni tu shirika hilo
lilipandisha gharama za huduma za umeme, ambazo hata hivyo bado zinalalamikiwa
na wateja.
Alisema bei hiyo mpya, inaweza
kuwashtua wateja, lakini alisema ndio hali ya biashara na kwamba ZECO haina
jinsi zaidi ya kuridhia mabadiliko hayo.
Aliwataka wateja kutumia umeme kwa uangalifu ili kupunguza matumizi
yasiyo ya lazima.
Hivi karibuni, Mkurugenzi Mdhibiti Uchumi wa EWURA, Nd. Felix
Ngamlagosi,alitangaza rasmi ongezeko la gharama za umeme kwa asilimia 50
gharama ambazo zilianza kutumika rasmi Januari Mosi 2014.
Alisema Oktoba 11, mwaka jana TANESCO liliwasilisha maombi ya
kurekebisha bei ya umeme kwa Ewura na kupendekeza kuongeza bei kwa asilimia
67.87 kuanzia Oktoba 1, jana.
Alisema Tanesco pia iliomba
ongezeko la asilimia 12.74 kuanzia Januari 1, 2014 na asilimia 9.17 kuanzia
Januari 1, 2015.
Hali hiyo imefanya kundi la wateja wakubwa waliounganishwa katika
msongo wa juu, likiwamo Shirika la Umeme la Zanzibar (Zeco), umeme umepanda kwa
shilingi 53, kutoka shilingi 106 hadi shilingi 159 kwa uniti moja sawa na
ongezeko la asilimia 50.
Akizungumza na waandishi wa
habari juzi, Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO,Felchesmi Mramba, alisema TANESCO
inazidai taasisi za serikali kiasi cha shilingi
bilioni 129 kati ya hizo shilingi bilioni 70 ni deni la Zanzibar
No comments:
Post a Comment