Na Asya
Hassan
SHIRIKA
la Misaada ya Maendeleo la Marekani (USAID), limekabidhi baiskeli 123 na vifaa
vya kufundishia kwa wahudumu wa afya ya jamii wa Zanzibar ili ziweze kuwasaidia katika
harakati zao za kutoa huduma hiyo kwa mama wajawazito na watoto.
Hafla
hiyo iliyofanyika kituo cha afya Dunga wilaya ya kati Unguja, ambapo Mwakilishi
wa Mkurugenzi wa USAID Tanzania, Erick Mlanga na Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego
nchini Tanzania, Maryjane Lacoste walimkabidhi vifaa hivyo Katibu Mkuu wa
Wizara ya Afya, Dk. Mohammed Saleh Jidawi.
Katika
makabidhiano hayo, Dk. Jidawi, alisema juhudi zinazofanywa na Wizara ya Afya
Zanzibar kwa kushirikiana na USAID zina lengo la kuhakikisha Zanzibar inafikia lengo la millennia la kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto.
Alisema
mradi huo umeweza kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwaelimisha mama wajawazito
kwenda kuzalia hospitali na vituo vya afya na kuacha tabia ya kuzalia
majumbani.
Hata
hivyo, alisema baskeli na vifaa walivyokabidhiwa wahudumu wa afya ya jamii
zitawarahisishia katika kazi zao pale wanapokwenda kutoa huduma.
Alitumia
nafasi hiyo kuwashukuru USAID na Jhpiego kwa kuuwezesha mradi huo muhimu kwa
maendeleo ya wanawake na watoto.
Nae
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa USAID Tanzania, Erick Mlanga, alisema mradi huo
umewawezesha wanawake wengi kuwasaidia wanawake wezao ili kujifungua katika
mazingira salama.
Naye
Mkurugenzi Mkazi wa Jhpiego nchi Tanzania, Maryjane Lacoste, alisema kuanzia
mwaka 2008 watu wa Marekani kupitia mradi wa MAISHA wamekuwa wakishirikiana na
Serikali ya Zanzibar katika kuboresha afya ya
mama na mtoto katika vituo tisa vya afya Unguja na Pemba .
Nae
Mratibu wa afya ya uzazi ya mama na mtoto wilaya ya kati Unguja, Mwanamvua
Mussa, alisema katika shehia sita zilizomo kwenye, kulikuwa na maendeleo kwa
wanawake kujhifungulia vituo vya afya.
Kati ya
baiskeli hizo,72 zitagaiwa kwa wahudumu wa afya ya jamii wilaya ya Wete, Mkoani
na Micheweni Pemba na baiskeli 51 kwa wahudumu wa afya ya jamii wilaya ya kati na kaskazini
'A'.
No comments:
Post a Comment