Habari za Punde

Sheikh Arusha amwagia tindikali

Na Joseph Ngilisho, ARUSHA
SHEIKH wa msikiti wa Sawiyatu Qadiria,Hassan Bashiri (33) mkazi wa Tindigani,Unga Ltd jijini hapa, amejeruhiwa vibaya kwa kumwagiwa tindikali na watu wasiofahamika wakati akijerea nyumbani kwake usiku wa kuamkia leo.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani Arusha, Liberatus Sabas, tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana majira ya saa 3:45 usiku,ambapo Sheikh huyo alikuwa akitokea mjini  baada ya kuachana na wenzake wawili waliokuwa wakijadili masuala ya kikao cha maulid.

Alisema wakati akijerea nyumbani kwake alikutana na mtu mmoja aliyekuwa amesimama kwenye kiambaza cha msikiti na kumsalimia, hata hivyo alisema  hakumbuki iwapo alijibiwa, ila wakati akiendelea kutembea  alihisi kuna mtu anamfuata kwa nyuma.

“Wakati anaendelea kuelekea nyumbani kwake akahisi kuna mtu anamfuatilia na alipogeuka ili ajue ni nani anamfuatilia ndipo mtu huyo alimwagia kemikali  hicho kinachosadikiwa kuwa tindikali,” alisema.

Alisema mtu huyo baada ya kutimiza azma hiyo alitoweka kwa kutimua mbio na kuelekea kusikojulikana,hata hivyo askari waliokuwa doria maeneo ya karibu walipata taarifa na kuelekea eneo la tukio,ambapo walimkuta majeruhi huyo akiwa hajitambui.

Kwa mujibu wa Sabas polisi inamshikilia mtu mmoja kwa mahijiano kuhusiana na tukio hilo,wakati huo huo majeruhi amelazwa hospitali ya mkoa Mount Meru kwa ajili ya matibabu.


Matukio ya viongozi wa dini kujeruhiwa kwa tindikali yamekuwa maarufu ambapo Asheikh Saidi Makamba wa msikili wa Arumeru alijeruhiwa vibaya Julai 13 mwaka jana kabla ya Katibu wa Bakwata, Abdulkarimu Jonjo kulipuliwa kwa bomu Oktoba 24, 2012.

1 comment:

  1. Serekali na wapenda uzalendo wanapaswa kufanya upelelezi wa kina maana mji muhimu kama Arusha unakosa amani kwa sasa hasa kwa makasisi wa dini mbalimbali.

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.