Na Khamisuu
Abdallah
MTU mmoja
amefariki dunia baada ya jahazi lenye namba za usajili 111 walilokuwa
wakisafiria kuzama karibu na bahari ya kisiwa cha Chumbe.
Jahazi hilo
lililokuwa likitokea Zanzibar kuelekea Tanzania Bara na kubeba mizigo pamoja na
mabaharia watano, lilizama baada kutoka mbao na kujaa maji.
Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi, Kamishna wa Polisi, Mkadam Khamis Mkadam,
alimtaja marehemu kuwa ni Mohammed Khatib Mahadhi, ambae alikuwa ndie nahodha
wa jahazi hilo .
Kamanda
Mkadam alisema jahazi hilo
lilikuwa limepakia vitu mbali mbali vikiwemo televisheni na baiskeli.
Alisema maiti
ya nahodha huyo ilipatikana kando ya kisiwa cha Chumba usiku wa kuamkia jana
ikielea.
Alisema tukio
hilo lilitokea
Mei 18 mwaka huu majira ya saa 4:00 za usiku katika maeneo ya kisiwa cha Chumbe.
Aliwataja
walionusurika kuwa ni Juma Khatib Abdalla mkaazi wa Kiembesamaki, Habibu Haji
Mussa, Twaha Amin Haji, Amin Abdalla Khamis na Seif Hassan Juma ambao
hawakufamika mahala wanapoishi.
Aidha alisema
manusura wapo salama na wanaendelea na shughuli zao.
No comments:
Post a Comment