Na
Mwashamba Juma
SEKTA
ya kilimo imetajwa kuwa hatarini kuangamia kutokana na athari za mabadiliko ya
tabianchi yaliyosababisha maeneo mengi ya kilimo kuvamiwa na maji ya
bahari,jambo ambalo linahatarisha usalama wa chakula.
Makamu
wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad kwa niaba ya rais wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, alisema
hayo wakati akizundua mkakati wa mabadiliko ya tabianchi katika hoteli ya
Zanzibar Ocean View, Kilimani mjini, Unguja.
Alisena
maeneo yaliyoko kwenye ukanda wa pwani, chini ya mita tano kutoka usawa wa bahari
yako hatarini kuathirika kutokana na kuingia maji ya bahari kulikosababishwa na
kupanda kwa kina cha bahari.
Alisema
uchumi na maisha ya visiwa vya Zanzibar unaotegemea zaidi ustawi wa shughuli za
kilimo, mifugo, uvuvi, utalii na miundombinu, shughuli hizo ziko kwenye tishio
la kuathiriwa na mabaidiko ya tabianchi.
Alisema
mabadiliko ya tabianchi yameathiri mfumo wa mvua kwa sekta ya kilimo, hali
inayoathiri zaidi sekta hiyo pamoja na mazao kutokanana kukosekana mvua za
kutosha au zenye viwango vikubwa ambazo zinaathiri ustawi wa mazao ya kilimo.
Aidha
alisema jumla ya maeneo 148 yanayotegemewa kwa shughuli za kilimo yanaingia
maji ya chumvi kutokana na kupanda kwa kina cha bahari ambapo Pemba
123 na Unguja 25 ambapo sasa fursa yakilimo zinapatikana kwa tabu.
Alisema
mabadiliko ya tabianchi ni matokeo ya shughuli za wanaadamu za maisha yao ya
kila siku katika kujitafutia riziki, ikiwemo ukataji misitu ovyo, umwagaji wa
taka ngumu, uvuvi haramu na uchafu unaotokana na taka za wiwandani pamoja na
uchafuzi wa hewa unaotokana na hewa mkaa.
Alisema
kiasi cha hekta milioni 17 za ardhi kwa
mwaka zinageuka kuwa jangwa duniani kote sambamba na kiwango cha joto kuzidi
hadi nyuzi joto 4.5 ifikapo mwaka 2050 na kuongeza kuwa kina cha bahari
kinatarajiwa kupanda hadi kufikia ujazo wa bahari 2.2 kutokana na kukithiri kwa
joto kali.
Hivyo
Zanzibar kama sehemu ya dunia alisema ina wajibu
wa kuungana na nchi zote duniani kuadhimisha siku za mazingara kwa lengo la
kutafakari kwa kina matatizo ya kimazingira yanayoikabili sambamba na kutumia
fursa hiyo kuyatatua.
Alisema
mkakati wa mabadiliko ya tabianchi uliozinduliwa unatoa tathmini juu ya athari
za mabadiliko hayo pamoja na kubuni njia sahihi za kukabiliana na athari zake.
“Kimsingi
mkakati huu unatoa tathmini ya mabadiliko ya tabianchi kwa Zanzibar pamoja na
kutoa njia muhimu za kujihami na kukabiliana na athari hizo pamoja na kupunguza
fursa za kukabiliana na ongezeko la hewa ukaa,” alisema.
Akizungumzia
suala la utalii,alisema serikali ya Zanzibar
imeamua kuufanya utalii kuwa sekta kiongozi kwa uchumi wa Zanzibar kutokana na kuwa na vivutio vingi
ambavyo vina jumuisha mambo ya kale, historia, utamaduni na maliasili ambayo ni
misitu ya hifadhi, fukwe na bahari.
Alisema
vivutio hivyo vinaonekana kuathiriwa na mabadiliko ya tabianchi, sambamba na
hote nyingi zilizojengwa kabirbu na fukwe za bahari zinaonekana kuathiriwa na
mmong’onyoko wa fukwe.
Uzinduzi
wa mkakati wa mabadiliko ya tabianchi ulikwenda sambambana maadhimisho ya siku
ya mazingira duniani ambapo ujumbe wa mwaka huu unasema ‘Sema usikike, ongezeko
la kina cha bahari hakikubaliki.’
No comments:
Post a Comment