Na Fatina
Mathias, Dodoma
WAZIRI Mkuu, Mhe.
Mizengo Pinda, amesema serikali kwa kushirikiana vyombo vya usalama vya nje,
itahakikisha inawabaini watu wanaowashambulia
viongozi wa dini na watalii mjini Zanzibar .
Kauli hiyo
aliitoa jana alipokuwa akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Viti Maalum,
Betty Machangu (CCM) katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri
Mkuu.
Mbunge huyo
alitaka kujia hatua ambazo serikali imechukua
dhidi ya matukio ya mauaji hayo mjini Unguja.
“Hivi
karibuni tulishuhudia mauaji ya Padri kule Zanzibar, lakini pia tumeshuhudia
pia wawekezaji Wafaransa wakiuawa na maiti zao kutumbukizwa kwenye
kisima,lakini tumeshuhudia Masheikh na walimu wa kujitolea wakimwagiwa
tindikali, Waziri Mkuu matukio yote hayo serikali imechukua hatua
gani,”alihoji.
Pinda alisema serikali imejipanga vizuri kwa
kujaribu kushirikiana na vyombo vya nje ili kuendelea kuwabaini wahusika wa
matukio hayo ikiwa ni pamoja na vyanzo na sababu ili kuyakabili kabla
hayajatokea.
“Na kwa
taarifa nilizonazo hata baadhi ya matukio ambayo yalikuwa yafanyike tumeweza
kuyakabili kabla ya kutokea,hivyo niwahakikishie Watanzania na hata watalii kwa
ujumla kwamba hali kwa kweli ni shwari kwa ujumla wake na serikali
tumeshachukua hatua stahiki na tutaendelea kuwa macho zaidi kukabiliana na hali hii ambayo inajitokeza hapa na
pale,”alisema.
Katika swali
lake la msingi Machangu alihoji vikundi vya uharifu na kigaidi vilivyoibuka
mkoani Mtwara,Tanga,Iringa na Dar es
salaam .
Alitolea
mfano wa vikundi vya Dar es Salaam vya Kontau, Jenerali Nyau, Komando Yusuph,
Sure, Panya Road, Mbwa Mwitu, Kiboko
Msheli na waasi M23 ambavyo ni vikundi vya vijana wadogo wanaovamia wananchi mchana
na kuwaibia.
Alisema kwa
upande wa vikundi vya Tanga na Mtwara ni vikundi vya kigaidi ambavyo vilifichwa
msituni kupewa mafunzo ya kigaidi ambapo inasemekana wako vijana wanaopelekwa Somalia kwa
mafunzo zaidi ya kigaidi.
Pinda alikiri
kuibuka kwa vikundi hivyo na kusema mara nyingi tatizo hilo
linapotokea serikali huchukua hatua za haraka kujaribu kudhibiti tatizo hilo .
Aliwataka
vijana kujiepusha kujiingiza katika vitendo ambavyo baadaye vinaweza
vikawaingiza katika mgongano na vyombo vya dola.
Kuhusu
vikundi cha Mtwara, Pinda alisema jambo hilo
linawezekana japo hakuwa na taarifa hizo hivyo akamuomba Machangu kumpa muda
ili aweze kuzungumza na wahusika wa Mtwara ili kuweza kupata uhalisia wa tukio hilo .
Wakati huo
huo,Mbunge wa Musoma mjini, Vicent Nyerere, alimtaka Mhe. Pinda kutoa kauli ya
serikali katika kusuluhisha mgogoro wa ardhi kati ya wananchi wa Makoko Musoma
mjini na kikosi cha jeshi la Wananchi cha 27KJ.
Nyerere
alisema maeneo ya kambi za jeshi hayakuwa yamewekwa mipaka iliyokuwa
ikitambulika vizuri na wananchi na kwa sababu hayakuendelezwa kwa muda mrefu wananchi waliamua kuingia katika maeneo hayo huku
halmashauri kwa kujua ama kutokujua wakiwaacha
wakiendelea na shughuli zao.
Akijibu swali
hilo, Mhe. Pinda alisema vyombo vya ulinzi hasa Jenshi la Wananchi mara nyingi
hupangwa katika maeneo husika kutokana na sababu fulani za kiulinzi hivyo kama
eneo limechwa kwa muda mrefu na kuonekana halina matumizi lazima watu wataingia
katika eneo hilo
na kufanya shughuli zao.
“Kinachonisumbua mimi ni kwamba inakuwaje jeshi
ambalo mnatambua eneo lenu mngoje mpaka kaya 300 zijenge bado
hamjashituka,zimekamilika ndipo mnasema eneo letu mimi kidogo hilo linanisumbua,” alisema
No comments:
Post a Comment