Na Masanja
Mabula,Pemba
NAIBU Katibu
Mkuu wa CCM Zanzibar, Mhe.Vuai Ali Vuai, amewataka wanaCCM kutowafumbia macho viongozi wanaokwenda
kinyume na matakwa ya chama.
Kauli hiyo ameitoa
wakati akizungumza na baadhi ya viongozi wa sekretarieti za CCMo kuanzia ngazi
ya tawi, wadi, jimbo na wilaya wa wilaya ya Micheweni.
Alisema lengo
la CCM ni kudumisha amani, umoja na
mshikamano ndani na nje ya chama na kutaka kutowapa nafasi viongozi wanaojihusisha
na majungu kama wanataka kuimarisha chama.
"Wekeni
vikao vya mara kwa mara kujadili changamoto ndani ya chama kwa kushirikianaa
viongozi wa serikali kwani nao wanafanya kazi kutekeleza ilani ya CCM,”
alisema.
Aidha alisema
ushirikiano huo utasaidia kutengeneza njia itakayotumika kuleta ushindi katika
uchaguzi mkuu wa 2015.
Alisema
uimara wa CCM unategemea uimara na uhai
wa wanachama na jumuiya zake na kuwaomba viongozi hao kuwahimiza wanachama wa
chama hicho kulipia ada ili kukifanya chama kuendesha shughuli zake kwa
ufanisi.
"Tusingoje
wakati wa uchanguzi ili kulipia ada zetu
lengo ni kutaka kupata kura, hivyo tunatakiwa kujiwekea mipango ya kuhakikisha
kwamba kila mwananchama pamoja na jumuiya zake analipia kadi kwa wakati,” alisema.
Aliwataka
wanaCCM kukitendea haki chama chao kwa
kuhakikisha wanashiriki katika mchakato wa kupiga kura kupitisha rasmu ya katiba wakati utakapofika.
Mwenyekiti wa chama hicho mkoa wa kaskazini
Pemba, Mberwa Hamad Mberwa, alisema CCM mkoa huo wako pamoja na viongozi wa juu
wa chama na kwamba wanajianda kwa ajili kupiga kura ya maoni kuhusu katiba
mpya.
No comments:
Post a Comment