Mafundi kutoka ZECO wakiwa katika harakati za kutengeneza
panel iliyoleta hitilafu za umeme na kupelekea maeneo yote ya mji wa Unguja
kukosa umeme
Baada ya kukamilika kwa matengenezo
Kuamkia alfajiri ya leo ya tarehe 17/06/2014 maeneo yate
ya mji wa Unguja na maeneo jirani ya mji wa Unguja yalikumbwa na ukosefu wa
umeme uliotokea kuanzia majira ya saa 11 asubuhi hadi saa 7 mchana
kulikosababishwa na hitilafu zilizotokea katika moja ya panel zake na kuungua
kwa breaker katika kituo cha kusambazia umeme Mtoni mjini Unguja.
Katika kipindi hicho chote njia (laini) za maeneo ya mji wa Unguja zinazopokea umeme
wa mkondo wa 11kV yalikosa umeme. Njia (laini) hizo ni njia ya Mtoni-Mpendae, Cotex,
Saateni 5 na Saateni 6.
Miongoni mwa maeneo yaliyokosa umeme ni:
Laini ya Saateni 5: Saateni, Mkele, Muungano,
Jang’ombe, Mpendae, Kidongochekundu, Kilimani, Kikwajuni.
Laini ya Saateni 6: Mlandege, Darajani, Malindi,
Kiponda, Forodhani, Mkunazini, Gongoni, Mwembetanga, Shangani, Hospitali ya Mnazi
Mmoja.
Laini ya Cotex: Mwembemakumbi, Kwaalamsha,
Kariakoo, Mwembeshauri, Misufini, Maruhubi, Mabanda ya Ng’ombe, Mtoni, Beit el
Ras, Kibweni, Bububu, Mwanyanya, Dole, Kizimbani, Kinumoshi.
Laini ya Mtoni-Mpendae: Chumbuni, Makadara,
Darajabovu, Kilimahewa, Sebleni, Nyerere, Magogoni, Magomeni, Mwanakwerekwe,
Melinne Uzi, Kijitoupele, Kwarara, Nyarugusu, Fuoni, Chunga, Welezo, Kinuni,
Masingini, Kianga, Meli sita, Mwera, Koani, Kidimni, Dunga, Mgenihaji, Uzini,
Bambi, Pagali.
Tahadhari kwa wateja ni kwamba wakati wowote ule umeme
unapozimika ni vyema kuzima vifaa vya umeme vilivyowazi ili kuepuka athari ya
kuunguza vifaa vyao wakati umeme utakaporudi.
No comments:
Post a Comment