Habari za Punde

ZANLINK YAZINDUA UTAMBULISHO WA CHAPA YAKE MPYA


TAARIFA KWA AJILI YA VYOMBO VYA HABARI
                       
·        Yazindua nembo mpya, kauli mbiu na tovuti mpya.
·        Yatumia teknolojia mpya ya 4G Wimax.
·        Ya panga kuongeza usambazaji wa mkonge wake katika maeneo zaidi ya Zanzibar.
  
Zanlink kampuni inayoongoza katika utoaji wa huduma ya internet leo rasmi imezindua chapa yake mpya, ambayo inaashiriwa na utambulisho wa nembo mpya, kauli mbiu pamoja na tovuti yake mpya.Mabadiliko haya ni taswira ya maendeleo ambayo Zanlink imekuwa ikiyapata tangu ilipoanzishwa kiasi cha miaka 14 iliyopita.

Uzinduzi huu mpya ni uwakilishi mzuri wa biashara na mabadiliko ya Zanlink katika mtazamo wa malengo ya mbele, muonekano wake na ujumbe wake. Utambulisho huu mpya ni hatua madhubuti ya kuwafikishia taarifa wateja waliopo na wateja watakao kuja kuwa sisi tunaendelea kutoa huduma ambayo inawazidi washindani wetu. 

Utambulisho mpya wa Zanlink ni wa kisasa na unao waunganisha wateja katika hali ya kirafiki huku nembo yake ikiwa na herufi za “Z” na “L” ambazo kwa pamoja huweza kuifanya Zanlink itambulike kwa urahisi.

Chini ya mwamvuli huu mpya wa utambulisho, kampuni imeamua kuyatumia maneno “keeping you connected” kama kauli yake mbiu ambayo itatumika katika matangazo yake pamoja na katika shughuli zote za kuitambulisha Zanlink.

Kauli mbiu hii ni fupi lakini ni yenye kuelezea malengo na mtazamo wa Zanlink wakati huo huo unasisitiza jambo ambalo Zanlink hujitahidi kutekeleza kila siku kwa wateja wake.

Zanlink imechukua uwelekeo huu mpya kwa kuzindua upya tovuti yake iliyofanyiwa mabadiliko ya www.zanlink.com ambayo inaonesha taswira mpya ya Zanlink pamoja na huduma inazozitoa.

Tovuti hiyo imehusisha kwa kujumuisha vitu ambavyo vinataarifu sifa na huduma za Zanlink, pamoja na ufanisi wake, mazingatio na uhakika wa huduma. Tovuti hii  pia hutaarifu kuhusu uwajibikaji wa kampuni katika utoaji wa huduma zake na katika kuisaidia jamii kama ambavyo imekuwa ikifanya katika kipindi cha hivi karibuni.


Uzinduzi wa leo hauhusishi tu ubadilishwaji wa utambulisho wa muonekano wetu wa kama vile nembo, lakini pia unahusisha mabadiliko katika namna tunavyotoa huduma kwa wateja wetu.

Utambulisho mpya pekee hautoweza kuthibitisha uaminifu wetu katika utoaji wa huduma lakini tunaamini kwa dhati kuwa chapa yetu mpya itatuhamasisha katika mipango yetu endelevu katika kutoa huduma iliyo bora zaidi kwa wateja wetu  

Kuambatana na uzinduzi huu, kampuni imeanza kutoa huduma yake mpya ya teknolojia ya 4G WiMAX ambayo hutumika kwenye masafa ya 3.5 GHz ambayo ni masafa ya leseni na hivyo huduma itaweza kutolewa yenye uhakika zaidi na isiyoingiliana na masafa mengine.

Mipango ipo pia ambayo inafanyiwa kazi ya kuongeza mtandao wa kutumia mkonge katika maeneo zaidi ya Zanzibar. Mwanzoni mwaka huu, Zanlink ilikamilisha kuweka kituo Tanzania bara cha kutoa na kuunganisha huduma mbalimbali za “VLAN” na “Layer2”.


Kufanya haya yameipatia Zanlink wigo zaidi wa kujenga mashirikiano ya kimkakati pamoja na watoaji huduma wa kimataifa katika Afrika Mashariki.     

 Uzinduzi wa chapa yetu mpya ya utambulisho utaanzisha awamu mpya itakayozungumzia sisi ni nani kama kampuni. Tunajivunia kuwa mbele ya wenzetu katika sekta hii, na chapa yetu mpya ya utambulisho itaonesha umbali ambao Zanlink imetokea katika kipindi cha miaka 14 ya historia yake.

Tulianza kwa kutoa huduma kwa njia ya mawasiliano ya simu na tukakua na kuweza kuwafikia 65% ya wateja wote waliyomo katika soko kwa kutoa huduma mbalimbali zenye kuhitajiwa na wateja wetu. Wakati huo huo tukiendeleza utoaji huo wa huduma huku tukiwazingatia na kuwathamini wateja wetu kwa kuwahudumia katika viwango vya juu.

Chapa hii mpya tayari imeshaanza kutumika katika namna zote za electronik kama vile katika tovuti yetu, na pia katika mitandao ya kijamii na katika namna nyenginezo za mawasiliano ya electronik na katika chapa mbalimbali.

Kuhusu ZANLINK
Zanlink ilianzishwa mwaka 2000 na ni kampuni yenye kuongoza katika utoaji wa huduma Zanzibar kwa kutoa huduma ya “broadband” kwa kasi zaidi pamoja na huduma nyenginezo za kimtandao.
Zanlink imeweka mtandao wenye ubora wa hali ya juu ambao unajumuisha mtandao wa mkonge katika mji na pia mtandao wa kutumia mionzi ambao unasaidia utoaji wa huduma mbalimbali. Mtandao huu umesambaa katika maeneo mbalimbali ya Unguja na Pemba.
Zee Communications LTD (Zanlink)
S.L.P 4024, Zanzibar, Tanzania
Simu: + 255 24 2237480/1. Barua pepe: info@zanlink.com. URL: www.zanlink.com



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.