Habari za Punde

Amuua mama yake baada ya kumpikia magimbi badala ya ugali

Na Rose Chapewa, Mbeya
MWANAMME aliyefahamika kwa jina la Kiswigo Anganisye (33) mkazi wa kijiji cha Ibungila, anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumpiga fimbo mama yake mzazi  sehemu ya kichwani na usoni na kisha kumnyonga shingo na kusababaisha kifo chake,baada ya kumpikia magimbi badala ya ugali.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi, Ahmed Msangi, mwanamke  aliyeuawa ni Martha Kyando (73) mkazi wa kijiji cha Ibungila.

Alisema tukio hilo lilitokea Julai mosi mwaka huu  majira ya saa 6:30 usiku katika kitongoji cha Mpunguti kijiji cha Ibungila kata ya Malindo, tarafa ya Ukukwe wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.

Alisema chanzo cha mauaji hayo ni baada ya mama huyo kumpikia mtuhumiwa magimbi badala ya ugali, ambapo alichukia na kumpiga  mama yake.


Alisema  uchunguzi unaonesha mtuhumiwa huyo anasumbuliwa na ugonjwa wa akili, na kwamba bado uchunguzi zaidi unaendeea, ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yake.

Katika tukio jingine  watu wawili wanaodaiwa kuwa raia waMalawi wanashikiliwa kwa kosa la  kuingia nchini  bila kibali.


Aliwataja watu hao kuwa ni Thomas Juma (29) na Bonophace Chitete (29), na kwamba walikamatwa Julai 1 mwaka huu majira ya saa 5:15 wilayani Kyela baada ya jeshi hilo kufanya msako maalumu.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.