Na Abdi Suleiman, Pemba
BAADA ya huduma za upasuaji kusimama kwa
muda katika hospitali ya wilaya Chake Chake baada ya kuharibisha mashine ya dawa
ya usingizi,(anaesthetic machine), hatime huduma hizo zimerejea baada ya
mashine hiyo kongwe kutengenezwa.
Taarifa ya kuharibika mashine hiyo kwa
mara ya kwanza ilichapishwa katika ukurasa wa mbele wa gazeti hili.
Huduma hizo zilizosimama tokea Juni 20 na
kusababisha wagonjwa na wajawazito wanaohitaji kufanyiwa upasuaji kuhamishiwa
hospitali za Mkoani na Chake, zimeanza kurejea tena kuanzia Jumatatu ya wiki
hii.
Dk. Alawi Hamad Othman,alisema huduma
hiyo imerejea baada ya masheine hiyo kufanyiwa matengenezo na mafundi wa
wizara.
Hata hivyo, alisema mashine hiyo
imeshachoka na wakati wowote inaweza kuharibika tena.
“Baada ya wandishi kuandika habari ya
kuharibika mashine hii, fundi mkuu wa wizara alikuja na kuungana na fundi wa
hospitali yetu kuitengeneza na imekubali na sasa tunaendelea kutoa huduma kama
kawaida yetu, tunawashukuru (waandishi kwa kutusaidia),”alisema.
Mashine hiyo ambayo ni moja katika
hospitali hiyo inayohutumia wagonjwa kutoka wilaya nzima ya Wete, ipo
hospitalini hapo tokea 1992.
Baadhi ya wagonjwa waliofanyiwa upasuaji,
waliiomba serikali kuharakisha kupatikana mashine mpya.
Walisema kuharibika kwa mashine hiyo kumesababisha
mateso makubwa kwao.
Ali Khamis mume wa Mariyam Kambi,
aliyefanyiwa upasuaji, alisema walilazimika kukaa hospitali kwa muda wa wiki
moja kusubiri mashine hiyo itengenezwe huku mke wake wakiwa na maumivu makali
ya tumbo.
No comments:
Post a Comment