Habari za Punde

Mufti Simba awaonya wanaoteka misikiti

Na Joseph ngilisho, Arusha
MUFTI Mkuu wa Tanzania,  Shekh   Issa Bin Shaaban Simba, amewaonya Waislamu wanaosababisha migogoro misikitini na wakati mwengine kuteka viongozi wa misikiti.

Alitoa onyo hilo baada ya kutatua mgogoro wa uongozi katia mskiti mkuu uliopo Bondeni manispaa ya Arusha.

Alisema kuna baadhi ya Waislamu wamekuwa wakiitumia misikiti sehemu za migogoro na kupindia uongozi uliowekwa kisheria kwa sababu zao binafsi.

Alisema hali hiyo mbali ya kusababisha migogoro pia imeifanya misikiti kuwa na makundi mawili ya uongozi, jambo ambalo halikubaliki.

Alisema kutokana na hali hiyo amelazimika kufanya
ziara Mkoani Arusha na kukutana na viongozi wa serikali,viongozi wa  Bakwata wa makundi yote yanayokinzana, ili kujaribu kumaliza mvutano.


Mufti Simba, alisema viongozi waliokuwa wakishikilia msikiti huo hawana haki, badala yake wanaotakiwa kuwa viongozi ni  Sheikh wa mkoa, Shaban Juma Abdallah, Kaimu Katibu wa mkoa, Ustadhi Abdallah Masoud na Mwenyekiti wa halmashauri, Ustadhi Mohamed Juma Marawi.

Aidha alisema baraza la  Masheikh mkoa litaongozwa na  Sheikh Mwinshehe Mwinyimgeni,Sheikh Nassib Idd Nassib, Sheikh Hussein Said Ijunje,Sheikh Abdallah Hanafi Simba na Sheikh Abdulrahman Salum.

Aliwataja wajumbe wanostahili kuwepo kwenye halmashauri ya mkoa ni  Hassan Waziri Salum, Said Rashid Golugwa,Athuman Amir Yunus,Seif Juma Banka,Athuman Juma Luwuchu, Mohamed Kidange Laizer, Salim Rajab Majaaliwa na Rashid Kilavo Msuya.


Aliwahimiza Waislamu kuimarisha umoja na mshikamano kwa kuwa uislamu ni dini ya amani na sio ya mivutano.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.