Habari za Punde

Maalim Seif Atembelea Watoto Yatima wa Kituo cha Muzdalifa Zanzibar.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimiana na Mwekiti wa Jumuiya ya Kiislamu ya Muzdalifa wakati alipokwenda kuwatembelea Watoto Mayatima wanaohudumiwa na Jumuiya hio Amani Mjini Zanizbar.Katikati ni Katibu Mkuu wa Jumuiya Farouk Hamad.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akipokea Zawadi ya Mas-haf kwa mtoto Khunayna Said kwa niaba ya Wototo wenziwe Mayatima wanao hudumiwa na Muzdalifat alipowatembelea Makao Makuu ya Jumuia Amani Mjini Zanzibar.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamadi akipokea Zawadi kutoka kwa Katibu Mkuu wa Jumuiya yaKiislam ya  Muzdalifat Farouk Hamadi alipowatembelea Makao Makuu ya Jumuia Amani Mjini Zanzibar.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad kulia akimkabidhi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kiislamu ya Muzdalifa Abdalla Hadhar Bahasha yenye Sadaka kwa ajili ya Watoto yatima alipowatembelea watoto hao Makao Makuu ya Jumuia Amani Mjini Zanzibar.

Watoto Mayatima wanaohudumiwa na Jumuiya ya MUZDALIFAT wakisoma kasda kumkaribisha Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamadi alipowatembelea Makao Makuu ya Jumuia Amani Mjini Zanzibar.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad katikati akiwa pamoja na Viongozi wa Jumuia ya Kiislamu ya Muzdalifa wakiinua Mikono kuomba Dua kwa ajili ya Watoto na wote waliohudhuria alipowatembelea watoto yatima huko Makao Makuu ya Jumuia Amani Mjini Zanzibar.wakwanza kulia ni Katibu Mkuu wa Jumuiya  Farouk Hamadi na kushoto ni Mwenyekiti wa Jumuiya Abdalla Hadhar( Picha na Yussuf Simai Maelezo)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.