Habari za Punde

PBZ Yafutarisha Wateja Wake Pemba.

 MAKAMO wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe:Maalim Seif Sharif Hamad, akisalimiana na viongozi wa Benk ya watu wa Zanzibar, PBZ Tawi la Pemba wakati alipokuwa akiwasili katika futari maalumu iliyoandaliwa na Benk hiyo kwa wateja wake huko ZSSF Chake Chake Pemba.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, akiwa na Viongozi wa Serekali na wa PBZ, wakati wa futari Maalum ilioandaliwa na Benki ya Watu wa Zanzibar Ltd, kwa Wateja wake Kisiwani Pemba, iliofanyika katika viwanja vya Hoteli ya ZSSF Chakechake Pemba jana.
 Wananchi na Wafanyabiashara Kisiwani Pemba wakipata futari maalum ilioandaliwa na PBZ kwa ajili ya Wateja wao walioko Pemba na kujumuika na Wafanyakazi wa PBZ Tawi la Pemba, futari hiyo imefanyika katika viwanja vya hoteli ya ZSSF Chakechake Pemba jana. 
Wananchi wakipata futari maalum iliandaliwa na PBZ Tawi la Pemba katika viwanja vya hoteli ya ZSSF Pemba.
Mkurugenzi Mtendajin wa Benki ya Watu wa Zanzibar Ndg Juma Amour, akitowa shukrani kwa Wananchi na Wafanyabiasha wa Kisiwani Pemba baada ya kumaliza kupata futari ilioandaliwa kwa ajili yao katika viwanja vya hoteli ya ZSSF Chake Pemba na kuhudhuriwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamad.(Picha na Abdi Suleiman -Pemba)  

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.