Balozi wa
Hispania nchini Tanzania Mh. Luis Manuel Ceuesta Civis
(Kulia) akiongea na Makocha kutoka Timu ya Barcelona ya nchini Hispania
katika mkutano wa Wanahabari uliofanyika jijini Dar es Salaam jana (leo),
makocha hao wapo nchini kwa ajili ya kutoa mafunzo ya siku mbili kwa makocha
wazalendo, wa kwanza kushoto ni Kocha Daniel Bigas Alsina na katikati ni Kocha Isaac Oriol Guerrero
Hernandes
: Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya
Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi Juliana Yassoda
(Katikati) akiongea na Wanahabari (Hawapo pichani) kuhusu makocha wa Timu ya Barcelona kutoka nchini Hispania ambao wako nchini kwa ajili ya mafunzo ya makocha yatakayofanyika kwa muda
wa siku mbili, wa kwanza kulia ni Balozi wa Spain nchini Mh. Luis Manuel
Ceuesta Civis, mafunzo hayo yanatolewa kwa ushirikiano na Kiwanda cha Bia cha
Tanzania Breweries.
Kocha Isaac Oriol
Guerrero Hernandes (katikati) kutoka timu
ya Barcelona ya nchini Hispania (katikati) akitoa maelezo kwa wanahabari (hawapo
pichani) kuhusu mafunzo ya siku mbili watakayotoa kwa makocha 30 wakizalendo,
kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Bi. Juliana Yassoda
na wa kwanza kushoto ni kocha Kocha Daniel Bigas Alsina
Makocha wa Kizalendo 30 ambao wanatarajiwa kupewa mafunzo ya siku mbili kutoka
kwa makocha wa Barcelona wakiwa katika picha ya pamoja
Picha zote
na Benjamin Sawe kutoka Kitengo cha Mawasiliano Serikalini WHVUM
No comments:
Post a Comment