Na
Mwanajuma Mmanga
WANAFUNZI
7,503 wa darasa la saba kati ya wanafunzi 10,823 waliofanya mitihani ya
majaribio katika baadhi ya skuli za serikali za Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja,
wamefeli ambao ni sawa na asilimia 69.32.
Aidha
wanafunzi 1179 sawa na asilimia 9.82 hawakufanya mitihani hiyo.
Waliofaulu
kwa kiwango bora zaidi ni wanafunzi 39 tu sawa na asilimia 0.39, waliofaulu kwa
kiwango cha nzuri sana ni 362 sawa na asilimia 3.34 na waliofaulu kwa kiwango
cha nzuri ni 1468 sawa na asilimia 13.56 na waliofaulu kwa kiwango cha
inaridhisha ni 1451 sawa na asilimia 13.41.
Kwa
upande wa wanafunzi wa kidato cha pili, walioshindwa ni wanafunzi 8,144 sawa na
asilimia 84.772 kati ya wana 9,607
waliofanya mitihani hiyo.
Waliofaulu
kwa kiwango cha bora sana ni mwanafunzi mmoja sawa na asilimia 0.010, kiwango
cha nzuri sana ni wanafunzi 144 sawa na asilimia 1.499, waliofaulu kwa kiwango
cha nzuri ni 411 sawa na asilimia 4.278 na
waliofaulu kwa kiwango cha inaridhisha ni 906 sawa na asilimia 9.43.
Akitoa
tathmini ya ripoti ya matokeo hayo,Ofisa
Elimu Mkoa wa Mjini Magharibi,Khatibu Muhsin, wakati wa hafla ya utoaji wa
zawadi kwa wanafunzi bora waliofanya vizuri mitihani hiyo, iliyofanyika skuli
ya Skuli Haile Sellasie ikiwa ni sehemu ya sherehe ya kutimiza miaka 50 ya
elimu bila malipo, alisema
matokeo hayo hayaridhishi.
Akizungumzia
changamoto walizokabiliana nazo wakati wa ufanyaji wa mitihani hiyo, alisema ni
pamoja na mwamko mdogo kwa baadhi wazazi
katika uchangiaji wa fedha kwa ajili ya mitihani hiyo.
Pia
alisema kuwepo kwa utoro wa wanafunzi na ukosefu wa nyenzo za uchapishaji
mitihani, ilisababisha zoezi hilo kuwa gumu.
Alisema
inaonekana wanafunzi wanaofanya vizuri mitihani ya majaribio ndio wanaofaulu
mitihani ya taifa.
Alizitaja
skuli zilizoshiriki katika mitihani hiyo kuwa ni Kibweni, Wazazi Amani, Mkunazini, Chumbuni
Msingi, Kijichi, Mwenge, Mwanakwerekwe D na B, Kisiwandui na Kilimahewa.
Kwa
upande wa kidato cha pili ni Lumumba, Kiembesamaki,Vikokotoni, Benbella,
Kiponda, Tumekuja, Skuli ya Biashara Mombasa, Mikunguni, Mikindani Dole na
Mwanakwerekwe C.
Skuli
bora za msingi zilizofanya vizuri ni Wazazi, Mkunazini na kibweni na skuli za
sekondari ni Vikokotoni, Kiembesamaki na
Lumumba.
Mkuu
wa Mkoa Mjini Magharibi, Abdalla Mwinyi Khamis, aliwashauri walimu wakuu
kufanya mitihani kwa utaratibu unaoeleweka na kuepuka utitiri wa mitihani.
No comments:
Post a Comment