Habari za Punde

Mafunzo ya kupinga udhalilishaji wa kijinsia kwa walemavu yafanyika Pemba

 
MKURUGENZI Mtendaji wa Umoja wa watu wenye ulemavu UWZ, Zanzibar Rashid Ali Mohamed akielezea azma ya mradi wa kupinga udhalilishaji wa kijinsia, hasa kwa watu wenye ulemavu wa akili, kwenye mafunzo yaliofanyika ukumbi wa ZANZGOC Micheweni Pemba, kulia ni Msaidizi Naibu Katibu mkuu wa UWZ, Salim Abdalla Salim na katikati ni Afisa tawala wilaya ya Micheweni Ahmed Khalid, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

 
AFISA Mipango wa kituo cha huduma za sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, Khalifan Amour Mohamed akitoa mada juu ya vikwazo vilivyopo, katika kumaliza kesi za udhalilishaji wa kijinsia, kwenye mafunzo yaliondaliwa na UWZ yaliofanyika Micheweni, katikati ni sheha wa shehia ya Micheweni Dawa Juma Mshindo na kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Umoja wa watu wenye ulemavu UWZ, Zanzibar Rashid Ali Mohamed, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

 WASHIRIKI wa mafunzo ya kupinga udhalilishaji wa kijinsia hasa kwa watu wenye ulemavu wa akili yaliofanyika Micheweni na kuandaliwa na UWZ kwa kushirikiana na ZLSC na ZAFELA , (Picha na Haji Nassor, Pemba).

HAKIMU wa mahakama ya mkoa Chake Chake, Khamis Ali Simai akichangia maoni yake, kwenye mafunzo ya kupinga udhalilishaji wa kijinsia hasa kwa watu wenye ulemavu wa akili, yalioandaliwa na UWZ na kufanyika Micheweni Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.